< Yoshua 21 >

1 Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
Derpaa traadte Overhovederne for Leviternes Fædrenehuse frem for Præsten Eleazar og Josua, Nuns Søn, og Overhovederne for de israelitiske Stammers Fædrenehuse
2 Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
og talte saaledes til dem i Silo i Kana'ans Land: »HERREN bød ved Moses, at der skulde gives os nogle Byer at bo i med tilhørende Græsmarker til vort Kvæg.«
3 Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
Da afgav Israeliterne i Følge HERRENS Bud af deres Arvelod følgende Byer med Græsmarker til Leviterne.
4 Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
Loddet faldt først for Kehatiternes Slægter, saaledes at Præsten Arons Sønner blandt Leviterne ved Lodkastningen fik tretten Byer af Judas, Simeoniternes og Benjamins Stammer,
5 Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
mens de andre Kehatiter ved Lodkastningen efter deres Slægter fik ti Byer af Efraims og Dans Stammer og Manasses halve Stamme.
6 Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
Gersoniterne fik ved Lodkastningen efter deres Slægter tretten Byer af Issakars, Asers og Naftalis Stammer og Manasses halve Stamme i Basan.
7 Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
Merariterne fik efter deres Slægter tolv Byer af Rubens, Gads og Zebulons Stammer.
8 Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
Og Israeliterne afgav ved Lodkastning følgende Byer med Græsmarker til Leviterne, saaledes som HERREN havde paabudt ved Moses.
9 Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
Af Judæernes og Simeoniternes Stammer afgav de følgende ved Navn, nævnte Byer.
10 Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
Arons Sønner, der hørte til Kehatiternes Slægter blandt Levis Sønner — thi for dem faldt Loddet først — fik følgende:
11 Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
Man gav dem Anaks Stamfader Arbas By, det er Hebron, i Judas Bjerge, med omliggende Græsmarker;
12 Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
men Byens Mark og Landsbyer gav man Kaleb, Jefunnes Søn, i Eje.
13 Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
Præsten Arons Sønner gav man Hebron, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker, Libna med omliggende Græsmarker,
14 Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
Jattir med omliggende Græsmarker, Esjtemoa med omliggende Græsmarker,
15 Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
Holon med omliggende Græsmarker, Debir med omliggende Græsmarker,
16 Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
Asjan med omliggende Græsmarker, Jutta med omliggende Græsmarker og Bet-Sjemesj med omliggende Græsmarker; tilsammen ni Byer af de to Stammer;
17 Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
og af Benjamins Stamme Gibeon med omliggende Græsmarker, Geba med omliggende Græsmarker,
18 na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
Anatot med omliggende Græsmarker og Alemet med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer.
19 Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
Præsternes, Arons Sønners, Byer udgjorde i alt tretten Byer med omliggende Græsmarker.
20 Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
Kehatiternes Slægter af Leviterne, de øvrige Kehatiter, fik de Byer af Efraims Stamme, som tildeltes dem ved Lodkastning.
21 Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
Man gav dem Sikem, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker i Efraims Bjerge, Gezer med omliggende Græsmarker,
22 na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
Kibzajim med omliggende Græsmarker og Bet-Horon med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
23 Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
og af Dans Stamme Elteke med omliggende Græsmarker, Gibbeton med omliggende Græsmarker,
24 Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
Ajjalon med omliggende Græsmarker og Gat-Rimmon med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
25 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
og af Manasses halve Stamme Ta'anak med omliggende Græsmarker og Jibleam med omliggende Græsmarker; tilsammen to Byer;
26 Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
i alt ti Byer med omliggende Græsmarker tilfaldt de øvrige Kehatiters Slægter.
27 Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
Blandt Leviternes Slægter fik fremdeles Gersoniterne af Manasses halve Stamme Golan i Basan, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker og Asjtarot med omliggende Græsmarker; tilsammen to Byer;
28 Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
og af Issakars Stamme Kisjjon med omliggende Græsmarker, Daberat med omliggende Græsmarker,
29 Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Jarmut med omliggende Græsmarker og En-Gannim med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
30 Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
og af Asers Stamme Misj'al med omliggende Græsmarker, Abdon med omliggende Græsmarker,
31 Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Helkat med omliggende Græsmarker og Rehob med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
32 Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
og af Naftalis Stamme Kedesj i Galilæa, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker, Hammot-Dor med omliggende Græsmarker og Kartan med omliggende Græsmarker; tilsammen tre Byer;
33 Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
Gersoniternes Byer efter deres Slægter udgjorde i alt tretten med omliggende Græsmarker.
34 Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
De øvrige Leviter, Merariternes Slægter, fik af Zebulons Stamme Jokneam med omliggende Græsmarker, Karta med omliggende Græsmarker,
35 Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
Rimmona med omliggende Græsmarker og Nahalal med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
36 Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
og hinsides Jordan over for Jeriko af Rubens Stamme Bezer i Ørkenen paa Højsletten, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker, Jaza med omliggende Græsmarker.
37 na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
Kedemot med omliggende Græsmarker og Mefa'at med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
38 Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
og af Gads Stamme Ramot i Gilead, en af Tilflugtsbyerne for Manddrabere, med omliggende Græsmarker, Mahanajim med omliggende Græsmarker,
39 Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
Hesjbon med omliggende Græsmarker og Ja'zer med omliggende Græsmarker; tilsammen fire Byer;
40 Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
Byerne, der ved Lodkastningen tilfaldt de øvrige Levitslægter, Merariterne efter deres Slægter, udgjorde i alt tolv.
41 Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
Levitbyerne inden for Israeliternes Ejendom udgjorde i alt otte og fyrretyve med omliggende Græsmarker.
42 Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
Disse Byer skulde hver for sig have de omliggende Græsmarker med; det gjaldt for alle disse Byer.
43 Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
Saaledes gav HERREN Israel hele det Land, han havde tilsvoret deres Fædre at ville give dem, og de tog det i Besiddelse og bosatte sig der.
44 Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
Og HERREN gav dem Ro rundt om, ganske som han havde tilsvoret deres Fædre, og ingen iblandt deres Fjender kunde holde Stand over for dem; alle deres Fjender gav HERREN i deres Haand.
45 Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.
Ikke eet af alle de gode Ord, HERREN havde talet til Israels Hus, faldt til Jorden; alle sammen gik de i Opfyldelse.

< Yoshua 21 >