< Yoshua 19 >

1 Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
La segunda suerte salió para Simeón, para la tribu de los hijos de Simeón, según sus familias, que recibieron su herencia en medio de la herencia de los hijos de Judá.
2 Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
Su herencia fue Bersabee, Seba, Moladá,
3 Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
Hazersual, Balá, Esem,
4 Elitoladi, Bethuli na Horma.
Eltolad, Betul, Horma,
5 Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
Siclag, Betmarcabot, Hazersusá,
6 Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
Betlebaot y Sarunen: trece ciudades con sus aldeas.
7 Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Ayin, Rimón, Éter y Asan: cuatro ciudades con sus aldeas;
8 Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
y todas las aldeas de los alrededores de estas ciudades, hasta Balaatbeer, que es Rama del Sur. Esta fue la herencia de la tribu de los hijos de Simeón, según sus familias.
9 Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
La herencia de los hijos de Simeón se tomó de la porción de los hijos de Judá, porque la porción de los hijos de Judá era demasiado grande para ellos; por tanto, los hijos de Simeón obtuvieron su herencia en medio de la herencia de ellos.
10 Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
La tercera suerte salió para los hijos de Zabulón según sus familias. La frontera de su herencia se extendía hasta Sarid.
11 Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
Subía su frontera hacia el oeste, a Maralá, y tocaba en Dabéset, y también en el torrente que pasa frente a Jocneam.
12 Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
De Sarid se volvía al este, hacia donde nace el sol, hasta el territorio de Kislot-Tabor, salía a Deberat, y subía a Jafía.
13 Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
De allí pasaba hacia el este, hacia donde nace el sol, a Gathéfer, a Etiasín, dirigiéndose hacia Rimón, Metoar y Neá.
14 Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
La frontera daba la vuelta, por la parte del norte, hasta Hanatón, y terminaba en el valle de Jefteel.
15 Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
(Se le dio) también Catat, Nahalal, Simrón, Idalá y Betlehem: doce ciudades con sus aldeas.
16 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta fue la herencia de los hijos de Zabulón, según sus familias: estas ciudades con sus aldeas.
17 Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
La cuarta suerte salió para Isacar, para los hijos de Isacar, según sus familias.
18 Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
Su territorio era: Jesreel, Kesulot, Sunem,
19 Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
Hafaraim, Sión, Anaharat,
20 Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
Rabit, Kisión, Ebes,
21 Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
Rémet, Enganim, Enhadá y Betfasés;
22 Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
la frontera tocaba en el Tabor, Sahasimá y Betsemes, y su territorio terminaba en el Jordán: dieciséis ciudades con sus aldeas.
23 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta fue la herencia de la tribu de los hijos de Isacar, según sus familias: las ciudades con sus aldeas.
24 Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
La quinta suerte salió para la tribu de los hijos de Aser, según sus familias.
25 Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
Su territorio comprendía: Helcat, Halí, Beten, Acsaf,
26 Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
Alamelec. Amad y Misal. Tocaba al oeste en el Carmelo y en Sihor-Libnat.
27 Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
Volviéndose hacia oriente, hasta Betdagón, tocaba en Zabulón y en el valle de Jefteel, por la parte del norte, pasaba por Bet-Emec y Neiel; y se extendía hacia Cabul, por la izquierda,
28 Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
y Hebrón, Rohob, Hamón y Cana, hasta Sidón, la grande.
29 Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
La frontera torcía hacia Ramá, hasta la plaza fuerte de Tiro, se volvía hacia Hosá, para terminar en el mar, en el distrito de Acsib.
30 Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
También Umá, Afec y Rohob: veinte y dos ciudades con sus aldeas.
31 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta fue la herencia de la tribu de los hijos de Aser, según sus familias: estas ciudades con sus aldeas.
32 Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
La sexta suerte salió para los hijos de Neftalí, para los hijos de Neftalí según sus familias.
33 Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
Comenzaba su territorio desde Hélef, desde el encinar de Zaananim, e iba por Adaminékeb y Jabneel hasta Lacum, acabando en el Jordán.
34 Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
Luego torcía la frontera hacia el oeste hasta Asnot-Tabor, y pasando de allí a Hucoc, lindaba con Zabulón, por el sur, tocando a Aser por el oeste, y a Judá del Jordán, en el este.
35 Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
Las ciudades fuertes eran Sidim, Ser, Hamat, Racat, Kinéret,
36 Adama, Rama, Hazori,
Adamá, Rama, Hasor,
37 Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
Kedes, Edreí, En- Hasor,
38 Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
Jirón, Migdalel, Hórem, Betanat, y Betsemes: diez y nueve ciudades con sus aldeas.
39 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Esta fue la herencia de la tribu de los hijos de Neftalí, según sus familias: las ciudades con sus aldeas.
40 Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
La séptima suerte salió para la tribu de los hijos de Dan, según sus familias.
41 Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
El territorio de su herencia comprendía: Zorá, Estaol, Irsemes,
42 Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
Saalabin, Ayaón, Itlá,
43 Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
Elón, Timná, Acarón,
44 Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
Eltequé, Gibetón, Baalat,
45 Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
Jehud, Beneberac, Gatrimón,
46 Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
Mejarcón y Racón, con el territorio de enfrente de Joppe.
47 Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
El territorio de los hijos de Dan era demasiado estrecho para ellos, por lo cual los hijos de Dan subieron y pelearon contra Lésem; la conquistaron y la pasaron a filo de espada; y tomándola en posesión habitaron allí; llamando a Lésem, Dan, según el nombre de su padre Dan.
48 Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Esta fue la herencia de la tribu de los hijos de Dan, según sus familias: estas ciudades con sus aldeas.
49 Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
Después de terminar la distribución del país, según sus territorios, los hijos de Israel dieron a Josué, hijo de Nun, una posesión en medio de ellos.
50 Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
Por orden de Yahvé le dieron la ciudad que él había solicitado, a saber, Timnatsérah, en la montaña de Efraím; y reedificó la ciudad y habitó allí.
51 Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Estas son las herencias que el sacerdote Eleazar, Josué, hijo de Nun, y las cabezas de las casas paternas de las tribus de los hijos de Israel repartieron por sorteo, en Silo, ante Yahvé, a la entrada del Tabernáculo de la Reunión, terminando así la distribución del país.

< Yoshua 19 >