< Yoshua 19 >

1 Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni na waligawiwa kwa kila ukoo wao. Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.
Второто жребие излезе за Симеона, за племето на Симеоновците според семействата им; и наследството им беше всред наследството на юдейците.
2 Urithi waliokuwa nao ni Beerisheba, Sheba, Molada,
За своето наследство те имаха; Вирсавее (или Савее), Молада,
3 Hazari Shuali, Bala, Ezemu,
Асур-суал, Вала, Асем,
4 Elitoladi, Bethuli na Horma.
Елтолад, Ветул, Хорма,
5 Simoni alikuwa pia na Ziklagi, Bethi Markabothi, Hazari Susa,
Сиклаг, Вет-маркавот, Асарсуса,
6 Bethi Lebaothi, na Sharuheni. Kulikuwa na miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. Vile vile
Ветловаот и Саруен; тринадесет града със селата им;
7 Simoni alimiliki Aini, Rimon, Etheri, na Ashani. Hii ilikuwa ni miji minne pamoja na vijiji vyake.
Аин, Римон, Етер и Асан; четири града със селата им;
8 Miji hii pamoja na vijiji vilivyoizunguka hata kufika Baalathi Beeri (ambao ndio Rama katika Negevu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simoni, waliopewa kwa koo zao.
и всичките села, които бяха около тия градове, до Ваалат-вир (който е южният Рамат). Това е наследството за племето на симеонците според семействата им.
9 Urithi wa kabila la Simoni ulikuwa sehemu ya himaya ya kabila la Yuda. Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda ilikuwa ni kubwa kwao, na hivyo kabila la Simoni lilipokea urithi wao kutoka katika sehemu yao ya katikati.
От дяла на юдейците се даде наследството на симеонците, защото делът на юдейците беше голям за тях; за това, симеонците наследиха дял всред тяхното наследство.
10 Upigaji wa kura ya tatu uliangukia kwa kabila la Zabuloni, na walipewa kwa koo zao. Mpaka wa urithi wao ulianzia huko Saridi.
Третото жребие излезе за завулонците, според семействата им; и пределът на наследството им беше до Сарид;
11 Mpaka wao ulipanda upande wa magharibi kuelekea Marala na ukaigusa Dabeshethi, na kisha ukasonga kuelekea kijito kilichokuwa mkabala na Yokineamu.
и границата им отиваше западно до Марала, и досягаше Давасес и досягаше потока, който е срещу Иокнеам;
12 Kutoka Saridi mpaka ulizunguka upande wa mashariki kuelekea mashariki na ulienda hadi mpaka wa Kislothi Tabori. Kutoka hapo uliendelea hadi Daberathi na kisha ulipanda hata Yafia.
и от Сарид завиваше към изгрева на слънцето до междата на Кислот-тавор, и излизаше на Даврат, и възлизаше на Яфия,
13 Kutoka hapo ulipita katika upande wa mashariki mwa Gathi Heferi, na kisha ukafika Ethikazini, baadaye ulienda hadi Rimoni na kisha ukageuka kuelekea Nea.
и от там минаваше към изток в Гетефер, в Ита-касин, и излизаше в Римон-метоар към Нуя;
14 Mpaka ulizunguka kueleka kaskazini ukafika Hanathoni na ulikomea katika bonde la Ifta Eli.
и от север границата завиваше в Анатот, и свършваше в долината Ефтаил,
15 Mkoa huu ulijumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala, na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
като включваше Катат, Наадал, Симрон, Идала и Витлеем, дванадесет града със селата им.
16 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni, waliopewa kwa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Това е наследството на завулонците по семействата им, -тия градове със селата им.
17 Upigaji kura wa nne uliangukia kwa Isakari, na waligawiwa kufuatana na koo zao.
Четвъртото жребие излезе за Исахара, за исахарците по семействата им.
18 Eneo lao lilijumuisha Jezreelli, Kesuloothi, Shunemu,
Пределът им беше Езраил, Кесулот, Сунам,
19 Hafaraimu, Shioni, na Anaharathi.
Афераим, Сеон, Анахарат,
20 Pia ilijumuisha miji ya Rabithi, Kishioni, Ebezi,
Равит, Кисион, Авес,
21 Remethi, Enganimu, Enihada, na Bethipazezi.
Ремет, Енганим, Енада и Вет-фасис;
22 Mpaka wao ulifika Tabor, Shahazuma, na Bethi Shemeshi, na ukakomea katika Yordani. Ilikuwa ni miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
и границата досягаше Тавор, Сахасима и Ветсемес; и границата им свършваше при Иордан; шестнадесет града със селата им.
23 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari, na walipewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Това е наследството за племето на исахарците по семействата им, - градовете със селата им.
24 Upigaji wa kura ya tano uliangukia kwa kabila la Asheri, na walipewa kwa koo zao.
Петото жребие излезе за племето на асирците семействата им.
25 Eneo lao lilijumuisha miji ya Helikathi, Hali, Beteni, Akashafu,
Пределът им беше Хелкат, Али, Ветен, Ахсаф,
26 Alameleki, Amadi, na Mshali. Mpaka wa magharibi ulitanuka hadi Karmeli na Shihori Libnathi.
Аламелех, Амад и Мисал, и достигаше, до Кармил на запад и до Сихор-ливнат;
27 Kisha ulizunguka upande wa mashariki kueleka Bethi Dagoni na ukaenda hadi Zabuloni, na kisha ukafika katika bonde la ifutaheli, upande wa kaskazini mwa Bethemeki na Neieli. Baadaye uliendelea mbele hata Kabuli kueleka upande wa Kaskazini.
и границата им завиваше към изгрева на слънцето при Вет-дагон, и досягаше Завулон и долината Ефтаил на север от Ветемек и Наил, и излизаше при Хаул на ляво,
28 Na kisha ulienda hadi Ebroni, Rehobu, Hammoni, na Kana, hata kufika mji mkubwa wa Sidoni.
и Еврон, Роов, Амон и Кана, до големия Сидон;
29 Mpaka ulirudi nyuma kuelekea Rama, na kisha ukafika kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Baada ya hapo mpaka ulizunguka kuelekea Hosa na ulikomea katika bahari, katika mkoa wa Akizibu,
и границата завиваше към Рама и към укрепения град Тир; и границата завиваше към Оса, и свършваше при морето край страната на Ахзив,
30 Umma, Afeki, na Rehobu. Kulikuwa na miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
и Ама, Афен и Роов; двадесет идва града със селата им.
31 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri, na waliopewa kwa koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Това е наследство за племето на асирците по семействата им - тия градове със селата им.
32 Upigaji wa kura wa mara ya sita uliangukia kwa kabila la Nafutali, na walipewa kufuatana na koo zao.
Шестото жребие излезе за нефталимците, за нефталимците по семействата им.
33 Mpaka wao ulianzia Helefu, kutoka katika mwaloni huko Zaananimu, ulipanda hadi Adaminekebu na Yabneeli, umbali kama Lakumu; na ulikomea katka Yordani.
Границата им беше от Елеф, от Алон близо при Саананим, и Адами-некев, и Явнеил, до Лакум и свършваше при Иордан;
34 Mpaka ule ulizunguka upande wa magharibi kuelekea Aznothi Tabori na ulipanda hadi Hukoki; uligusa Zabuloni katika upande wa kusini, na ulifika hata Asheri katika upande wa magharibi, na Yuda katika upande wa mashariki huko katika mto Yordani.
и границата завиваше към запад до Азнот-тавор, и от там излизаше при Укок, и досягаше Завулон на юг, а досягаше Асир на запад и Юда при Иордан към изгрева на слънцето.
35 Miji yenye ngome ilikuwa ni Zidimu, Zeri, Hammathi, Rakathi, Kinnerethi,
А укрепените градове бяха: Сидим, Сер, Амат, Ракат Хинерот,
36 Adama, Rama, Hazori,
Адама, Рама, Асор,
37 Kedeshi, Edrei, na Eni Hazori.
Кедес, Едран, Енасор,
38 Pia kulikuwa na miji ya Yironi, Migdaleli, Horemu, Bethi Anathi, na Bethi Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa, pamoja na vijiji vyake.
Ирон, Мигдалил, Орам, Ветанат и Ветсемес; деветнадесет града със селата им,
39 Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali, na walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao.
Това е наследството за племето на нефталимците по семействата им - градовете със селата им.
40 Upigaji wa kura ya saba uliangukia kwa kabila la Dani, na walipewa kufuatana na koo zao.
Седмото жребие излезе за племето на данците по семействата им.
41 Eneo lao la urithi lilijumuisha miji ya Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi,
Пределът, който те наследяваха, беше Саара, Естаол, Ерсемес,
42 Shaalabini, Aijaloni, na Ithila.
Салавим, Еалон, Етла,
43 Vile vile lilijumuisha miji ya Eloni, Timna, Ekroni,
Елон, Тамната, Акарон,
44 Eliteke, Gibethoni, Baalathi,
Елтеко, Гиветон, Ваалат,
45 Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni,
Юд, Вани-варак, Гетримон,
46 Me -Yarkoni, na Rakoni sambamba na eneo la karibu na Yopa.
Меиаркон и Ракон, с околността, която е срещу Иопа,
47 Ilitokea wakati mpaka wa kabila la Dani ulipowapotea, kabila la Dani waliishambulia Leshemu, wakapigana nao, na wakauteka. Waliua kila mtu kwa upanga, wakauchukua ukawa mali yao, na wakakaa ndani yake. Wakauita mji ule Dani jina la babu yao badala ya Leshemu.
А пределът на данците не им стигаше; за това данците отидоха и воюваха против Лесем, и като го превзеха и го поразиха с острото на ножа, взеха го за притежание и заселиха се в него; и Лесем наименуваха Дан, по името на праотца си Дан.
48 Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani, waliopewa kufuatana na koo zao - miji pamoja na vijiji vyake.
Това е наследството за племето на данците по семействата им, - тия градове със селата им.
49 Walipomaliza kugawana urithi wa nchi, watu wa Israeli walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao.
А като свършиха подялбата на земята, според пределите й, израилтяните дадоха на Исуса Навиевия син наследството всред себе си;
50 Kwa amri ya Yahweh walimpatia mji wa Timnathi Sera ambao aliuomba, ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Aliujenga mji na akaishi huko.
според Господната заповед, дадоха му града, който поиска, сиреч, Тамнат-сарах в хълмистата част на Ефрема; и той съгради града и живееше в него.
51 Na huu ndio urithi ambao Eliazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli, waligawa kwa kupiga kura huko Shilo, mbele za Yahweh katika mlango wa hema la kukutania. Na hivyo wakamaliza kuigawa nchi.
Тия са наследствата, който свещеникът Елеазар и Исус Навиевия син и началниците на бащините домове на племената на израилтяните разделиха с жребие в Сило пред Господа, при входа на шатъра за срещане. Така свършиха подялбата на земята.

< Yoshua 19 >