< Yoshua 18 >

1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
Et toute l’assemblée des fils d’Israël se réunit à Silo, et ils y dressèrent la tente d’assignation; et le pays leur fut assujetti.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
Et il restait parmi les fils d’Israël sept tribus auxquelles on n’avait pas encore distribué leur héritage.
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
Et Josué dit aux fils d’Israël: Jusques à quand vous porterez-vous lâchement à aller prendre possession du pays que l’Éternel, le Dieu de vos pères, vous a donné?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Choisissez-vous trois hommes par tribu, et je les enverrai; et ils se lèveront, et ils parcourront le pays, et ils en feront le relevé selon la proportion de leur héritage, puis ils viendront vers moi.
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
Ils le diviseront en sept parts; Juda se tiendra dans ses limites au midi, et la maison de Joseph se tiendra dans ses limites au nord;
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
et vous ferez le relevé du pays en sept parts, et vous me l’apporterez ici; et je jetterai ici le sort pour vous devant l’Éternel, notre Dieu.
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
Mais il n’y a point de part pour les Lévites au milieu de vous, car la sacrificature de l’Éternel est leur héritage. Et Gad, et Ruben, et la demi-tribu de Manassé, ont reçu au-delà du Jourdain, vers le levant, leur héritage, que Moïse, serviteur de l’Éternel, leur a donné.
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
Et les hommes se levèrent et s’en allèrent; et Josué commanda à ceux qui s’en allaient faire le relevé du pays, disant: Allez et parcourez le pays, et faites-en le relevé, et revenez auprès de moi, et je jetterai ici le sort pour vous devant l’Éternel, à Silo.
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
Et les hommes s’en allèrent, et traversèrent le pays, et en firent le relevé dans un livre, en sept parts, selon les villes; puis ils vinrent vers Josué, au camp, à Silo.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
Et Josué jeta le sort pour eux, à Silo, devant l’Éternel, et Josué répartit là le pays aux fils d’Israël, selon leurs distributions.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
Et le sort tomba pour la tribu des fils de Benjamin, selon leurs familles. Et le territoire de leur lot leur échut entre les fils de Juda et les fils de Joseph.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
Et leur frontière, du côté du nord, partait du Jourdain; et la frontière montait à côté de Jéricho, vers le nord, et montait dans la montagne vers l’occident, et aboutissait au désert de Beth-Aven;
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
et la frontière passait de là à Luz, au côté méridional de Luz, qui est Béthel; et la frontière descendait à Ataroth-Addar, près de la montagne qui est au midi de Beth-Horon la basse.
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
– Et la frontière fut tracée, et elle faisait un détour du côté occidental vers le midi, depuis la montagne qui est en face de Beth-Horon, vers le midi, et aboutissait à Kiriath-Baal, qui est Kiriath-Jéarim, ville des fils de Juda. C’est là le côté de l’occident.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
– Et le côté méridional partait de l’extrémité de Kiriath-Jéarim; et la frontière sortait vers l’occident, et elle sortait vers la source des eaux de Nephtoah.
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
Et la frontière descendait jusqu’au bout de la montagne qui est en face de la vallée de Ben-Hinnom, qui est dans la vallée des Rephaïm, vers le nord, et elle descendait la vallée de Hinnom à côté de Jébus, au midi, et descendait à En-Roguel.
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
Et elle était tracée vers le nord, et sortait par En-Shémesh, et sortait à Gueliloth, qui est vis-à-vis de la montée d’Adummim, et descendait à la pierre de Bohan, fils de Ruben,
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
et passait au côté nord, qui est vis-à-vis d’Araba, et descendait à Araba.
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
Et la frontière passait à côté de Beth-Hogla, au nord; et la frontière aboutissait à la pointe de la mer Salée, vers le nord, à l’extrémité méridionale du Jourdain. C’est là la frontière du midi.
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
– Et le Jourdain formait la limite du côté de l’orient. Tel fut l’héritage des fils de Benjamin, selon ses frontières, à l’entour, selon leurs familles.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
Et les villes de la tribu des fils de Benjamin, selon leurs familles, étaient: Jéricho, et Beth-Hogla, et Émek-Ketsits,
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
et Beth-Araba, et Tsemaraïm, et Béthel,
23 Avimu, Para, Ofra,
et Avvim, et Para, et Ophra,
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
et Kephar-Ammonaï, et Ophni, et Guéba: douze villes et leurs hameaux;
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
– Gabaon, et Rama, et Beéroth,
26 Mizpe, Kefira, Moza,
et Mitspé, et Kephira, et Motsa,
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
et Rékem, et Jirpeël, et Thareala,
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
et Tséla, Éleph, et Jébus, qui est Jérusalem, Guibha, Kiriath: 14 villes et leurs hameaux. Tel fut l’héritage des fils de Benjamin, selon leurs familles.

< Yoshua 18 >