< Yoshua 18 >

1 Kisha kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika pamoja hapo Shilo. Walilijenga hema la kukutania hapo na waliishinda nchi mbele yao.
Then the whole assembly of the people of Israel met together at Shiloh. They set up the tent of meeting there and they conquered the land before them.
2 Kulikuwa na makabila saba miongoni mwa watu wa Israeli ambayo yalikuwa bado hayajapewa urithi wao.
There were still seven tribes among the people of Israel whose inheritance had not been assigned.
3 Yoshua aliwaambia watu wa Israeli, “Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?
Joshua said to the people of Israel, “How long will you put off going into the land that Yahweh, the God of your ancestors, has given you?
4 Chagueni ninyi wenyewe watu watatu kutoka katika kila kabila, na nitawatuma. Wataenda na kuipeleleza nchi juu na chini. Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi wao, na kisha watarudi kwangu.
Appoint for yourselves three men from each tribe, and I will send them out. They will set out and survey the land up and down. They will write out a description of it with a view to their inheritances, and then they will come back to me.
5 Wataigawanya nchi katika sehemu saba. Yuda itasalia katika eneo lao upande wa kusini, na nyumba ya Yusufu itaendelea katika himaya yao katika upande wa kaskazini.
They will divide it into seven sections. Judah will remain in their territory on the south, and the house of Joseph will continue in their territory in the north.
6 Mtaigawanya nchi katika sehemu saba na kisha mtaniletea maelezo hayo hapa kwangu. Nami nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh Mungu wetu.
You will describe the land in seven sections and bring the description here to me. I will cast lots for you here before Yahweh our God.
7 Walawi hana sehemu miongoni mwenu, kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao. Makabila ya Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapokea urithi wao ng'ambo ya Yordani. Huu ni urithi ambao Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa wao.
The Levites have no portion among you, for the priesthood of Yahweh is their inheritance. Gad, Reuben, and the half tribe of Manasseh have received their inheritance, beyond Jordan. This is the inheritance that Moses the servant of Yahweh gave them.”
8 Hivyo, watu waliinuka na wakaenda. Yoshua akawaamuru wale walioenda kuandika maelezo ya nchi, akisema, “Pandeni juu na mshuke chini katika nchi na andikeni maelezo kuhusu nchi na kisha mrejee kwangu. Nitapiga kura kwa ajili yenu hapa mbele za Yahweh huko Shilo.
So the men got up and went. Joshua commanded those who went to write the description of the land, saying, “Go up and down in the land and write a description of it and return to me. I will cast lots for you here before Yahweh at Shiloh.”
9 Watu walienda na walitembea juu na chini katika nchi na wakaandika maelezo kuihusu nchi hiyo juu ya gombo kwa miji yake katika sehemu saba, kwa kutaja miji, kila mmoja katika sehemu moja. Kisha wakarudi kwa Yoshua katika kambi huko Shilo.
The men left and walked up and down in the land and wrote a description of it in a scroll by its cities in seven sections, listing the cities in each section. Then they returned to Joshua in the camp at Shiloh.
10 Kisha Yoshua akapiga kura kwa ajili yao huko Shilo mbele za Yahweh. Na hapo Yoshua akaigawa nchi kwa watu wa Israeli, kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.
Then Joshua cast lots for them at Shiloh before Yahweh. It was there that Joshua assigned the land to the people of Israel, and to each was given his portion of the land.
11 Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao. Eneo la nchi waliyopewa lilikuwa kati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu.
The assignment of land for the tribe of Benjamin clan by clan. The territory of their assigned land was located between the descendants of Judah and the descendants of Joseph.
12 Katika upande wa kusini, mpaka wao ulianzia katika Yordani. Mpaka ulipanda hata sehemu ya juu kaskazini mwa Yeriko, na kisha ukapita katikati ya nchi ya milima upande wa magharibi. Huko ukafika hadi nyika ya Bethi Aveni.
On the north side, their border began at the Jordan. The border went up to the ridge north of Jericho, and then up through the hill country westward. There it reached the wilderness of Beth Aven.
13 Kutoka hapo mpaka ulipita upande wa kusini katika mwelekeo wa Luzi (sehemu ile ile inayoitwa Betheli). Kisha mpaka ukashuka chini hata Atarothi Adda, karibu na mlima uliolekea kusini mwa Bethi Horoni.
From there the border passed along south in the direction of Luz (the same place as Bethel). Then the border went down to Ataroth Addar, by the mountain that lies south of Beth Horon.
14 Kisha mpaka ukaendelea upande mwingine: katika upande wa magharibi uligeukia upande wa kusini, ulienda mbele kuukabili mlima ulio ng'ambo ya Bethi Horoni. Mpaka huu ulikomea huko Kiriathi Baali ( ambao ndio Kiriathi Yearimu), mji ambao ulikuwa ni wa kabila la Yuda. Na huu ndio ulikuwa ni mpaka katika upande wa magharibi.
The boundary then went in another direction: On the western side it turned toward the south, heading toward the mountain across from Beth Horon. This boundary ended at Kiriath Baal (that is, Kiriath Jearim), a city that belonged to the tribe of Judah. This formed the border on the western side.
15 Katika upande wa kusini, mpaka ulianzia nje tu ya Kiriathi Yearimu. Mpaka uliendelea kutoka Efroni hata chemichemi ya maji ya Neftoa.
The south side began just outside of Kiriath Jearim. The border went from there to Ephron, to the spring of the waters of Nephtoah.
16 Kisha mpaka ulishuka chini hadi mpaka wa mlima ambao ulikuwa mkabala ya bonde la Beni Hinomu, ambalo lililokuwa katika upande wa kaskazini mwishoni mwa bonde la Refaimu. Kisha ulishuka chini kuelekea bonde la Hinomu, sehemu ya kusini mwa mteremko wa Wayebusi, na uliendelea kushuka chini hadi Eni Rogeli.
The boundary then went down to the border of the mountain which was opposite the Valley of Ben Hinnom, which was at the northern end of the Valley of Rephaim. It then went down to the Valley of Hinnom, south of the slope of the Jebusites, and continued down to En Rogel.
17 Ulizunguka upande wa kaskazini, kuelekea mwelekeo wa Eni Shemeshi, na kutoka hapa ulienda hadi Gelilothi, ambao ulikuwa mkabala na mwinuko wa Adumimu. Kisha ulishuka chini kuelekea Jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
It turned northward, going in the direction of En Shemesh, and from there it went out to Geliloth, which was opposite the ascent of Adummim. Then it went down to the Stone of Bohan the son of Reuben.
18 Ulipita kuelekea upande wa kaskazini wa bega la Bethi Araba na chini kuelekea Araba.
It passed on to the north of the shoulder of Beth Arabah and down to the Arabah.
19 Mpaka ulipita hadi upande wa bega la kaskazini la Bethi Hogla. Mpaka ulikome katika ghuba ya kaskazini mwa Bahari ya Chumvi, katika upande wa kusini mwishoni mwa Yordani. Huu ulikuwa ni mpaka wa upande wa kusini.
The border passed on to the north shoulder of Beth Hoglah. The border ended at the north bay of the Salt Sea, at the southern end of the Jordan. This was the boundary on the south.
20 Yordani ulikuwa mpaka wake katika upande wa mashariki. Na huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini, na walipewa kwa kila ukoo wao, mpaka baada ya mpaka, kwa kuizunguka nchi yote.
The Jordan formed its border on the eastern side. This was the inheritance of the tribe of Benjamin, and it was given clan by clan, border after border, all around.
21 Kwa hiyo sasa miji ya kabila la Benyamini kufuatana na koo zao ilikuwa ni Yeriko,
Now the cities of the tribe of Benjamin, clan by clan, had these cities: Jericho, Beth Hoglah, Emek Keziz,
22 Bethi Hogla, Emeki Kezizi, Bethi Araba, Zemaraimu, Betheli,
Beth Arabah, Zemaraim, Bethel,
23 Avimu, Para, Ofra,
Avvim, Parah, Ophrah,
24 Kefari Amoni, Ofini, na Geba. Ilikuwa ni miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Kephar Ammoni, Ophni, and Geba. There were twelve cities, including their villages.
25 Kulikuwa pia na miji ya Gibeoni, Rama, Beerothi,
There were also the cities of Gibeon, Ramah, Beeroth,
26 Mizpe, Kefira, Moza,
Mizpah, Kephirah, Mozah,
27 Rekemu, Iripeeli, Tarala,
Rekem, Irpeel, Taralah,
28 Zela, Haelefu, Yebusi (ambao ndio Yerusalemu), Gibea, na Kiriathi. Kulikuwa na miji kumi na nne, pamoja na vijiji vyake. Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini kufuatana na koo zao.
Zelah, Haeleph, Jebus (the same as Jerusalem), Gibeah, and Kiriath. There were fourteen cities, including their villages. This was the inheritance of Benjamin for their clans.

< Yoshua 18 >