< Yoshua 15 >

1 Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
La parte que le tocó en suerte a la tribu de los hijos de Judá, según sus familias, iba hacia el límite de Edom, hacia el desierto de Zin al extremo sur.
2 Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
Su límite por el lado sur iba desde la costa del mar Salado, desde la bahía que mira hacia el sur,
3 Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
y seguía por el sur hacia la subida de Acrabim, pasaba hasta Zin, subía por el sur de Cades Barnea y pasaba por Hebrón, y después de subir por Adar, volvía a Carca.
4 Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
De allí pasaba a Asmón y seguía hasta el arroyo de Egipto, y terminaba en el mar. Éste les será el límite del sur.
5 Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
El límite oriental era el mar Salado hasta la desembocadura del Jordán. El límite del norte era desde la costa del mar en la desembocadura del Jordán,
6 Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
y el lindero subía a Bet-hogla, pasaba al norte de Bet-arabá y subía hasta la piedra de Bohán, hijo de Rubén.
7 Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
El lindero subía después desde el valle de Acor hasta Debir, y por el norte volvía hacia Gilgal, que se encuentra frente a la subida de Adumim, situada al lado sur del valle. Después el límite pasaba por las aguas de En-semes, y terminaba en En-rogel.
8 kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
El lindero subía por el valle del hijo de Hinom, en el lado sur de donde estaban los jebuseos, es decir, Jerusalén, y subía a la cumbre de la montaña que está delante del valle de Hinom hacia el occidente, en el extremo norte del valle de Refaim.
9 Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
Desde la cumbre de la montaña el límite volvía hasta la fuente de las aguas de Neftoa, y salía a las ciudades de la montaña Efrón, luego rodeaba a Baala, la cual es Quiriat-jearim.
10 Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
De Baala el límite giraba al occidente hasta la montaña Seír, y pasaba por la ladera de la montaña Jearim, por el norte, que es Quesalón, y descendía a Bet-semes, y pasaba a Timná.
11 Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
Después la línea partía hacia la ladera de Ecrón, al norte, y giraba hacia Sicrón y después de pasar por la montaña Baala, salía a Jabneel, y el límite terminaba en el mar.
12 Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
El límite occidental era el mar Grande. Estos son los límites alrededor de los hijos de Judá, según sus familias.
13 Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
Pero a Caleb, hijo de Jefone, le dio su porción entre los hijos de Judá, conforme a la Palabra de Yavé [dada] a Josué, la ciudad de Arba, padre de Anac, la cual es Hebrón.
14 Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
Caleb echó de allí a tres de los hijos de Anac: a Sesai, Aimán y Talmai, descendientes de Anac.
15 Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
De allí subió contra los habitantes de Debir. Antiguamente el nombre de Debir era Quiriat-séfer.
16 Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
Entonces Caleb dijo: Al que ataque a Quiriat-sefer, y la conquiste, le daré a mi hija Acsa como esposa.
17 Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
Otoniel, hijo de Cenaz, hermano de Caleb, la conquistó. Y él le dio como esposa a su hija Acsa.
18 Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
Aconteció que cuando la llevaba, él la incitó a que pidiera a su padre un campo. Ella desmontó del asno, por lo cual Caleb le dijo: ¿Qué quieres?
19 Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
Ella entonces respondió: Dame una bendición. Porque me diste una tierra de sequedal, dame también fuentes de agua. Y él le dio las fuentes de arriba y las fuentes de abajo.
20 Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
Esta es la heredad de la tribu de los hijos de Judá, según sus familias.
21 Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
Las ciudades en el extremo sur de la tribu de los hijos de Judá, hacia el límite de Edom, fueron Cabseel, Eder, Jagur,
22 Kina, Dimona, Adada,
Cina, Dimona, Adada,
23 Kadeshi, Hazor, Ithinani,
Cedes, Hazor, Itnán,
24 Zifu, Telemu, Bealothi.
Zif, Telem, Bealot,
25 Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
Hazor-hadata, Queriot, Hesrón (que es Hazor),
26 Amamu, shema, Molada,
Amam, Sema, Molada,
27 Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
Hazar-gada, Hesmón, Bet-pelet,
28 Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
Hazar-sual, Beerseba, Bizotia,
29 Baala, Limu, Ezemu,
Baala, Lim, Esem,
30 Eltoladi, Kesili, Horma,
Eltolad, Quesil, Horma,
31 Ziklagi, Madimana, Sansana,
Siclag, Madmana, Sansana,
32 Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
Lebaot, Silim, Aín y Rimón: 29 ciudades con sus aldeas.
33 Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
En la llanura: Estaol, Sora, Asena,
34 Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
Zanoa, Enganim, Tapúa, Enam,
35 Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
Jerimut, Adulam, Soco, Azeca,
36 Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
Saraim, Aditaim, Gedera y Gederotaim: 14 ciudades con sus aldeas.
37 Zena, Hadasha, Migidagadi,
Zenán, Hadasa, Migdal-gad,
38 Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
Dileán, Mizpa, Jocteel,
39 Lakishi, Bozikathi, Egloni.
Laquis, Boscat, Eglón,
40 Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
Cabón, Lahmam, Quitlis,
41 Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
Gederot, Bet-dagón, Naama y Maceda: 16 ciudades con sus aldeas.
42 Libna, Etheri, Ashani,
Libná, Eter y Asán,
43 Ifuta, Ashina, Nezibu,
Jifta, Asena y Nezib,
44 Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
Queila, Aczib y Maresa: nueve ciudades con sus aldeas.
45 Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
Ecrón con sus villas y sus aldeas.
46 kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
Desde Ecrón hasta el mar, todas las que están junto a Asdod, con sus aldeas.
47 Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
Asdod, sus villas y sus aldeas. Gaza, sus villas y sus aldeas hasta el río de Egipto y el mar Grande, con su territorio.
48 Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
En la región montañosa: Samir, Jatir, Sucot,
49 Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
Dana, Quiriat-sana, que es Debir,
50 Anabu, Eshitemo, Animu,
Anab, Estemó, Anim,
51 Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
Gosén, Holón y Gilo: 11 ciudades con sus aldeas.
52 Arabu, Duma, Ehani,
Arab, Duma, Esán,
53 Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
Janum, Bet-tapúa, Afeca,
54 Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
Humta, Quiriat-arba, que es Hebrón, y Sior: nueve ciudades con sus aldeas.
55 Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
Maón, Carmel, Zip, Juta,
56 Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
Izreel, Jocdeam, Zanoa,
57 Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
Caín, Gabaa y Timná: diez ciudades con sus aldeas.
58 Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
Halhul, Bet-sur, Gedor,
59 Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
Maarat, Bet-anot y Eltecón: seis ciudades con sus aldeas.
60 Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
Quiriat-baal, que es Quiriat-jearim, y Rabá: dos ciudades con sus aldeas.
61 Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
En el desierto: Bet-arabá, Midín, Secaca,
62 Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
Nibsán, la Ciudad de la Sal, y En-guedi: seis ciudades con sus aldeas.
63 Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.
Pero los hijos de Judá no pudieron echar a los jebuseos que habitaban en Jerusalén. Así que los jebuseos viven con los hijos de Judá en Jerusalén hasta hoy.

< Yoshua 15 >