< Yoshua 15 >

1 Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
And the lot of the tribe of the children of Judah according to their families was: to the border of Edom, the wilderness of Zin, southward, in the extreme south.
2 Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
And their southern border was from the end of the salt sea, from the tongue that turns southward;
3 Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
and it went out south of the ascent of Akrabbim, and passed on to Zin, and went up on the south of Kadesh-barnea, and passed to Hezron, and went up toward Addar, and turned toward Karkaah,
4 Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
and passed on to Azmon, and went out by the torrent of Egypt; and the border ended at the sea. That shall be your border southward.
5 Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
— And the eastern border was the salt sea as far as the end of the Jordan. — And the border on the north side was from the tongue of the salt sea, at the end of the Jordan;
6 Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
and the border went up toward Beth-hoglah, and passed north of Beth-Arabah; and the border went up to the stone of Bohan, the son of Reuben;
7 Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
and the border went up toward Debir from the valley of Achor, and turned northward to Gilgal, which is opposite to the ascent of Adummim, which is on the south side of the torrent; and the border passed to the waters of En-shemesh, and ended at En-rogel;
8 kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
and the border went up to the valley of the son of Hinnom, toward the south side of the Jebusite, that is, Jerusalem; and the border went up to the top of the mountain that is before the valley of Hinnom westward, which is at the end of the valley of Rephaim northward;
9 Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
and the border reached along from the top of the mountain toward the spring of the waters of Nephtoah, and went out toward the cities of mount Ephron; and the border reached along to Baalah, that is, Kirjath-jearim;
10 Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
and the border turned from Baalah westwards toward mount Seir, and passed toward the side of Har-jearim, that is, Chesalon, northwards, and went down to Beth-shemesh, and passed Timnah.
11 Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
And the border went out to the side of Ekron northwards, and the border reached along toward Shicron, and passed mount Baalah, and went toward Jabneel; and the border ended at the sea.
12 Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
— And the west border is the great sea and [its] coast. This is the border of the children of Judah round about, according to their families.
13 Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
And to Caleb the son of Jephunneh he gave a portion among the children of Judah according to the commandment of Jehovah to Joshua, the city of Arba, the father of Anak, that is, Hebron.
14 Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
And thence Caleb dispossessed the three sons of Anak, Sheshai and Ahiman and Talmai, who were born of Anak.
15 Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
And from there he went up against the inhabitants of Debir; now the name of Debir before was Kirjath-sepher.
16 Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
And Caleb said, He that smites Kirjath-sepher and takes it, to him will I give Achsah my daughter as wife.
17 Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
And Othniel the son of Kenaz, the brother of Caleb, took it; and he gave him Achsah his daughter as wife.
18 Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
And it came to pass as she came, that she urged him to ask of her father a field; and she sprang down from the ass. And Caleb said to her, What wouldest thou?
19 Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
And she said, Give me a blessing; for thou hast given me a southern land; give me also springs of water. Then he gave her the upper springs and the lower springs.
20 Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
This is the inheritance of the tribe of the children of Judah according to their families.
21 Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
The cities at the extremity of the tribe of the children of Judah, toward the border of Edom in the south, were: Kabzeel, and Eder, and Jagur,
22 Kina, Dimona, Adada,
and Kinah, and Dimonah, and Adadah,
23 Kadeshi, Hazor, Ithinani,
and Kedesh, and Hazor, and Jithnan,
24 Zifu, Telemu, Bealothi.
Ziph, and Telem, and Bealoth,
25 Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
and Hazor-hadattah, and Kerioth-Hezron, that is Hazor,
26 Amamu, shema, Molada,
Amam, and Shema, and Molada,
27 Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
and Hazar-gaddah, and Heshmon, and Beth-Pelet,
28 Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
and Hazar-Shual, and Beer-sheba, and Biziothiah;
29 Baala, Limu, Ezemu,
Baalah, and Ijim, and Ezem,
30 Eltoladi, Kesili, Horma,
and Eltolad, and Chesil, and Hormah,
31 Ziklagi, Madimana, Sansana,
and Ziklag, and Madmannah, and Sansanna,
32 Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
and Lebaoth, and Shilhim, and Ain, and Rimmon: all the cities twenty-nine, and their hamlets.
33 Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
— In the lowland: Eshtaol, and Zoreah, and Ashnah,
34 Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
and Zanoah, and En-gannim, Tappuah and Enam,
35 Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
Jarmuth and Adullam, Sochoh and Azekah,
36 Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
and Shaaraim, and Adithaim, and Gederah, and Gederothaim: fourteen cities and their hamlets.
37 Zena, Hadasha, Migidagadi,
Zenan, and Hadashah, and Migdal-Gad,
38 Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
and Dilean, and Mizpeh, and Joktheel,
39 Lakishi, Bozikathi, Egloni.
Lachish, and Bozkath, and Eglon,
40 Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
and Cabbon, and Lahmas, and Chithlish,
41 Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
and Gederoth, Beth-Dagon, and Naamah, and Makkedah: sixteen cities and their hamlets.
42 Libna, Etheri, Ashani,
Libna, and Ether, and Ashan,
43 Ifuta, Ashina, Nezibu,
and Jiphthah, and Ashnah, and Nezib,
44 Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
and Keilah, and Achzib, and Mareshah: nine cities and their hamlets.
45 Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
Ekron and its dependent villages and its hamlets.
46 kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
From Ekron and westward all that are by the side of Ashdod, and their hamlets.
47 Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
Ashdod, its dependent villages and its hamlets; Gazah, its dependent villages and its hamlets, as far as the torrent of Egypt, and the great sea and [its] coast.
48 Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
— And in the hill-country: Shamir, and Jattir, and Sochoh,
49 Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
and Dannah, and Kirjath-sannah, that is, Debir,
50 Anabu, Eshitemo, Animu,
and Anab, and Eshtemoh, and Anim,
51 Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
and Goshen, and Holon, and Giloh: eleven cities and their hamlets.
52 Arabu, Duma, Ehani,
Arab, and Dumah, and Eshan,
53 Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
and Janum, and Beth-Tappuah, and Aphekah,
54 Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
and Humtah, and Kirjath-Arba, that is, Hebron, and Zior: nine cities and their hamlets.
55 Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
Maon, Carmel, and Ziph, and Jutah,
56 Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
and Jizreel, and Jokdeam, and Zanoah,
57 Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
Kain, Gibeah and Timnah: ten cities and their hamlets.
58 Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
Halhul, Beth-Zur, and Gedor,
59 Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
and Maarath, and Beth-anoth, and Eltekon: six cities and their hamlets.
60 Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
Kirjath-Baal, that is, Kirjath-jearim, and Rabbah: two cities and their hamlets.
61 Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
— In the wilderness: Beth-Arabah, Middin, and Secacah,
62 Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
and Nibshan, and Ir-Hammelah, and En-gedi: six cities and their hamlets.
63 Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.
But as for the Jebusites, the inhabitants of Jerusalem, the children of Judah could not dispossess them; and the Jebusites dwell with the children of Judah at Jerusalem to this day.

< Yoshua 15 >