< Yoshua 12 >

1 Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao watu wa Israeli walishindwa. Waisraeli walichukua miliki ya nchi katika upande wa mashariki mwa Yordani sehemu ambako jua huchomoza, kutoka bonde la Mto Arnoni hadi Mlima Hermoni, na nchi yote ya Araba kuelekea kusini.
A oto królowie ziemi, których pobili synowie Izraela i posiedli ich ziemię za Jordanem na wschodzie, od rzeki Arnon aż do góry Hermon, i całą równinę na wschodzie:
2 Sihoni, mfalme wa Waamori, aliishi katika Heshiboni. Alitawala kutoka Aroeri, ambayo iko juu ya bonde la Arnoni kutoka katikati ya bonde, na nusu ya Geleadi kushuka mpaka Mto Yaboki katika mpaka wa Waamori.
Sichon, król Amorytów, który mieszkał w Cheszbonie, a panował od Aroeru, [leżącego] nad brzegiem rzeki Arnon, i od połowy tej rzeki oraz połowy Gileadu aż do rzeki Jabbok, granicy synów Ammona;
3 Sihoni pia alitawala juu ya Araba mpaka Bahari ya Kinerethi, kwenda mashariki, kuelekea Bahari ya Araba (Bahari ya Chumvi) upande wa mashariki, hadi huko Bethi Yeshimothi na upande wa kusini, kuelekea chini ya miteremko wa Mlima Pisiga.
A od równin aż do morza Kinneret na wschodzie, i aż do Morza Równiny, czyli Morza Słonego, na wschód, w kierunku Bet-Jeszimot, i od południa pod górę Pisga.
4 Ogu, mfalme wa Bashani, mmoja kati ya mabaki ya Rephaimu, aliyeishi huko Shatarothi na Edrei.
I obszar Oga, króla Baszanu, który pozostał z Refaitów i mieszkał w Asztarot i w Edrei;
5 Alitawala juu ya Mlima Hermoni, Saleka, na Bahani yote, hadi mpaka wa watu wa Geshuri na Wamakathi, na nusu ya Gleadi, hadi kufika mpaka wa Sihohi, mfalme wa Heshboni.
Panował on na górze Hermon, i w Salce oraz w całym Baszanie aż do granic Geszurytów i Maakatytów i nad połową Gileadu, granicą Sichona, króla Cheszbonu.
6 Musa mtumishi wa Yahweh, na watu wa Israeli walikuwa wamewashinda, na Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa nchi kama mali ya Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.
Pobił ich Mojżesz, sługa PANA, wraz z synami Izraela. I Mojżesz, sługa PANA, dał tę ziemię w posiadanie Rubenitom i Gadytom, i połowie pokolenia Manassesa.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambayo Yoshua na watu wa Israeli waliwashinda katika upande wa magharibi mwa mto Yordani, kutoka Baali Gadi katika bonde karibu na Lebanoni hadi Mlima Halaki karibu na Edom. Yoshua aliyapa nchi makabila ya Israeli ili yaimiliki.
A oto królowie ziemi, których pobili Jozue i synowie Izraela po zachodniej stronie Jordanu, od Baal-Gad w dolinie Libanu aż do góry Chalak, która wznosi się ku Seirowi, a których obszar Jozue dał pokoleniom Izraela w posiadanie według ich przydziałów;
8 Aliwapa nchi ya milima, tambarare, Araba, sehemu za milima, nyika na Negevu, nchi ya Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
Na górach, na równinach, na polach, na nizinach, na pustyni i na południowej ziemi; [ziemie] Chetytów, Amorytów, Kananejczyków, Peryzzytów, Chiwwitów i Jebusytów.
9 Wafalme hawa walikuwa ni mfalme wa Yeriko, mfalme wa Ai iliyo karibu na Betheli,
Król Jerycha – jeden; król Aj, które [jest] obok Betel – jeden.
10 mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Enaimu,
Król Jerozolimy – jeden; król Hebronu – jeden.
11 mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi,
Król Jarmutu – jeden; król Lakisz – jeden.
12 mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,
Król Eglonu – jeden; król Gezer – jeden.
13 mfalme wa Debiri, mfalme wa Gederi,
Król Debir – jeden; król Gederu – jeden.
14 mfalme wa Horima, mfalme wa Aradi,
Król Chormy – jeden; król Aradu – jeden.
15 mfalme wa Libna, mfalme wa Adula,
Król Libny – jeden; król Adullam – jeden.
16 mfalme wa Makeda, mfalme wa Betheli,
Król Makkedy – jeden; król Betel – jeden.
17 mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi,
Król Tappuach – jeden; król Cheferu – jeden.
18 mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni,
Król Afek – jeden; król Laszaronu – jeden.
19 mfalme wa Madoni, mfalme wa Hazori,
Król Madonu – jeden; król Chasoru – jeden.
20 mfalme wa Shimroni - Meroni, mfalme wa Akshafu.
Król Szimron-Meronu – jeden; król Achszafu – jeden.
21 mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido,
Król Tanaku – jeden; król Megiddo – jeden.
22 mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Jokineamu katika Karmeli,
Król Kedeszu – jeden; król Jokneamu z Karmelu – jeden.
23 mfalme wa Dori katika Nafutali Dori, mfalme Goyimu katika Giligali, na
Król Doru z krainy Dor – jeden; król narodów z Gilgal – jeden.
24 mfalme Tiriza. Hesabu ya wafalme ilikuwa ni thelathini na moja kwa ujumla wake.
Król Tirsy – jeden. Wszystkich królów było trzydziestu jeden.

< Yoshua 12 >