< Yoshua 1 >

1 Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
And it was after [the] death of Moses [the] servant of Yahweh and he said Yahweh to Joshua [the] son of Nun [the] servant of Moses saying.
2 “Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
Moses servant my he has died and therefore arise pass over the Jordan this you and all the people this into the land which I [am] about to give to them to [the] people of Israel.
3 Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
Every place which it will tread [the] sole of foot your on it to you I have given it just as I spoke to Moses.
4 kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
From the wilderness and Lebanon this and to the river great [the] river of Euphrates all [the] land of the Hittites and to the sea great [the] setting of the sun it will be territory your.
5 Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
Not he will stand anyone before you all [the] days of life your just as I was with Moses I will be with you not I will abandon you and not I will leave you.
6 Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
Be strong and be bold for you you will cause to inherit the people this the land which I swore to fathers their to give to them.
7 Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
Only be strong and be bold exceedingly to take care to do according to all the law which he commanded you Moses servant my may not you turn aside from it right and left so that you may prosper in every where you will go.
8 Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
Not it will depart [the] book of the law this from mouth your and you will meditate on it by day and night so that you may take care to do according to every [thing] written in it for then you will make successful ways your and then you will be successful.
9 Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
¿ Not have I commanded you be strong and be bold may not you be terrified and may not you be dismayed for [is] with you Yahweh God your in every where you will go.
10 Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
And he commanded Joshua [the] officers of the people saying.
11 “Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
Pass - in [the] midst of the camp and command the people saying prepare for yourselves food for in yet - three days you [are] about to pass over the Jordan this to go to take possession of the land which Yahweh God your [is] about to give to you to take possession of it.
12 Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
And to the Reubenite[s] and to the Gadite[s] and to [the] half of [the] tribe of Manasseh he said Joshua saying.
13 “Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
Remember the word which he commanded you Moses [the] servant of Yahweh saying Yahweh God your [is] giving rest to you and he will give to you the land this.
14 Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
Wives your little one[s] your and livestock your they will remain in the land which he gave to you Moses on [the] other side of the Jordan and you you will pass over arrayed for battle before brothers your all [the] mighty [men] of strength and you will help them.
15 Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
Until that he will give rest Yahweh - to brothers your like you and they will take possession of also they the land which Yahweh God your [is] about to give to them and you will return to [the] land of possession your and you will take possession of it which - he gave to you Moses [the] servant of Yahweh on [the] other side of the Jordan [the] rising of the sun.
16 Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
And they answered Joshua saying all that you have commanded us we will do and to every where you will send us we will go.
17 Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
According to all that we listened to Moses so we will listen to you only may he be Yahweh God your with you just as he was with Moses.
18 Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.
Every person who he will rebel toward mouth your and not he will obey words your to all that you will command him he will be put to death only be strong and be bold.

< Yoshua 1 >