< Yohana 9 >

1 Wakati, kama Yesu alipokuwa akipita, alimwona mtu kipofu tangu kuzaliwa kwake.
In gredoč mimo, ugleda človeka, kteri je bil slep od rojstva.
2 Wanafunzi wake wakamwuliza, “Rabi, nani aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu?”
In vprašajo ga učenci njegovi, govoreč: Rabi, kdo je grešil, ta ali roditelji njegovi, da se je slep rodil?
3 Yesu akawajibu, “Siyo huyu mtu wala wazazi wake waliotenda dhambi, bali kazi za Mungu zipate kufunuliwa kupitia kwake.
Jezus odgovorí: Ne ta ni grešil, ne roditelji njegovi; nego da se razodenejo dela Božja na njem.
4 Tunapaswa kufanya kazi zake yeye aliyenituma wakati bado ni mchana. Usiku waja wakati ambapo hakuna atakayeweza kufanya kazi.
Jaz moram delati dela tega, kteri me je poslal, dokler je dan; prišla bo noč, ko ne bo nihče mogel delati.
5 Wakati niwapo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”
Dokler sem na svetu, luč sem svetu.
6 Baada ya Yesu kusema maneno haya, alitema kwenye ardhi, alifanya tope kwa mate, na akampaka yule mtu machoni na lile tope.
Rekši to, pljune na zemljo, in napravi blato od sline, in pomaže z blatom slepcu očí.
7 Akamwambia, nenda kaoge katika kisima cha Siloam (Inayotafsiriwa kama 'aliyetumwa').” Kwa hiyo huyo mtu alienda, akanawa, na akarudi, anaona.
In reče mu: Pojdi, umij se v kopeli Siloamskej (kar se tolmači: Poslan). Ter odide in se umije, in vrne se videč.
8 Majirani wa yule mtu na wale waliomuona mwanzo kama mwombaji walisema, Je! huyu siye yule mtu aliyekuwa akikaa na kuomba?” wengine walisema, “Ni yeye.”
A sosedje, in kteri so ga bili poprej videli, da je slep, govorili so: Ali ni ta tisti, ki je sedel in prosil?
9 Na wengine walisema, “Hapana, bali anafanana naye.” Lakini alikuwa akisema, “Ni mimi.”
Nekteri so pravili: On je; drugi pa: Podoben mu je. On je pravil: Jaz sem.
10 Wakamwambia, “Sasa macho yako yalifunguliwaje?”
Rekó mu torej: Kako so ti se odprle očí?
11 Alijibu, mtu aitwaye Yesu alifanya tope na kupaka macho yangu na kuniambia, 'Nenda Siloam ukanawe.' Kwa hiyo nilienda, na nikanawa, na nikapata kuona tena.”
On odgovorí in reče: Človek, ki se imenuje Jezus, napravil je blato, in pomazal mi je očí, in rekel mi je: Pojdi v kopel Siloamsko, in umij se. In ko sem odšel, in sem se umil, spregledal sem.
12 Wakamwambia, “Yuko wapi?” Alijibu, “Sijui.”
Pa mu rekó: Kje je on? Reče: Ne vém.
13 Wakampeleka yule mtu aliyewahi kuwa kipofu kwa Mafarisayo.
Peljejo ga k Farizejem, tega, ki je nekedaj slep bil.
14 Nayo ilikuwa siku ya Sabato wakati Yesu alipotengeneza tope na kuyafumbua macho yake.
Bila je pa sobota, ko je Jezus blato napravil in mu odprl oči.
15 Ndipo tena Mafarisayo wakamwuliza alipataje kuona. Aliwaambia, “Aliweka tope katika macho yangu, nikanawa, na sasa naweza kuona.”
In vpraševali so ga zopet tudi Farizeji, kako je spregledal. On jim pa reče: Blato mi je del na oči, in umil sem se, ter vidim.
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hajatoka kwa Mungu kwa sababu haishiki Sabato.” Wengine walisema, “Inawezekanaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo?” Kwa hiyo kukawa na mgawanyiko kati yao.
Tedaj so nekteri od Farizejev govorili: Ta človek ni od Boga, ko sobote ne sveti. Drugi so govorili: Kako more grešen človek takošne čudeže delati? In bil je razpor med njimi.
17 Ndipo walipomwuliza yule kipofu tena, “Unasemaje juu yake kwa sababu aliyafungua macho yako?” Kipofu akasema, “Ni nabii.”
Zopet rekó slepcu: Kaj ti praviš za-nj, da ti je odprl očí? On pa reče: Da je prerok.
18 Hata wakati huu Wayahudi hawakumwamini kwamba alikuwa kipofu naye amepata kuona mpaka walipowaita wazazi wake yeye aliyepata kuona.
Judje pa niso verovali za-nj, da je slep bil in je spregledal, dokler niso roditeljev tega, ki je spregledal, poklicali,
19 Waliwauliza wazazi, Je, huyu ni mtoto wenu mnayesema alizaliwa kipofu? amewezaje sasa kuona?”
In jih vprašali, govoreč: Je li ta sin vaš, za kogar pravite, da se je slep rodil? Kako pa sedaj vidi?
20 Hivyo wazazi wake wakamjibu, “Tunajua kuwa huyu ni mtoto wetu na kwamba alizaliwa kipofu.
Odgovoré jim roditelji njegovi in rekó: Vémo, da je ta sin naš, in da se je slep rodil;
21 Jinsi gani sasa anaona, hatujui, na yeye aliyemfumbua macho yake, hatumjui. Mwulizeni yeye. Ni mtu mzima. Anaweza kujieleza mwenyewe.”
Kako pa sedaj vidi, ne vemo; ali kdo mu je oči odprl, mi ne vemo. On ima leta; njega vprašajte, on bo sam govoril za-se.
22 Wazazi wake walisema mambo haya, kwa sababu waliwaogopa Wayahudi. Kwa vile Wayahudi walikuwa wamekubaliana tayari kuwa, ikiwa yeyote atakiri kuwa Yesu ni Kristo, atatengwa na Sinagogi.
To so rekli roditelji njegovi za to, ker so se bali Judov; kajti Judje so se bili uže dogovorili, da bodo vsakega, kdor ga bo pripoznal za Kristusa, izpahnili iz shajališča.
23 Kwa sababu hii, wazazi wake walisema, “Ni mtu mzima, mwulizeni yeye.”
Za to so roditelji njegovi rekli: Saj ima leta; njega vprašajte.
24 Kwa hiyo kwa mara ya pili, walimwita yule mtu aliyewahi kuwa kipofu na kumwambia, “Mpe Mungu utukufu. Tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
Tedaj drugoč pokličejo človeka, kteri je slep bil, in rekó mu: Daj Bogu hvalo; in vémo, da je ta človek grešnik.
25 Ndipo yule mtu alijibu, “Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui. Kitu kimoja ninachokijua: nilikuwa kipofu, na sasa ninaona.”
On pa odgovorí in reče: Če je grešnik, ne vém; samo vém, da sem slep bil, in sedaj vidim.
26 Ndipo walipomwambia, “Amekufanyia nini? Aliyafumbuaje macho yako?”
Rekó mu torej zopet: Kaj ti je storil? Kako ti je odprl očí?
27 Alijibu, “Nimekwishawaambia tayari, na nyinyi hamkusikiliza! Kwa nini mnataka kusikia tena? Nanyi hamtaki kuwa wanafunzi wake pia, sivyo?
Odgovorí jim: Povedal sem vam uže, in niste slišali; kaj hočete zopet slišati? Ali hočete tudi vi njegovi učenci postati?
28 Walimtukana na kusema, “Wewe ni mwanafunzi wake, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa.
Oni pa ga opsujejo, in rekó: Ti si njegov učenec; mi smo Mojzesovi učenci.
29 Tunajua kwamba Mungu alizungumza na Musa, lakini kwa huyu mtu, hatujui kule atokako.”
Mi vémo, da je z Mojzesom govoril Bog; za tega pa ne vémo, odkod je.
30 Yule mtu akajibu na kuwaambia, “Kwa nini, hili ni jambo la kushangaza, kwamba hamjui anakotoka, na bado ameyafumbua macho yangu.
Človek odgovorí in jim reče: To je pač res čudno, da vi ne véste, odkod je, in odprl mi je očí.
31 Tunajua kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini ikiwa mtu yeyote anamwabudu Mungu na hufanya mapenzi yake, Mungu humsikiliza.
Vémo pa, da grešnikov Bog ne posluša; nego če kdo spoštuje Boga, in voljo njegovo izpolnjuje, tega posluša.
32 Tangu kuanza kwa Ulimwengu haijawahi kamwe kusikiwa kwamba yeyote ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
Od vekomaj se ni slišalo, da bi bil kdo od rojstva slepemu očí odprl. (aiōn g165)
33 Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingelifanya chochote.”
Ko ta ne bi bil od Boga, ne bi mogel ničesar storiti.
34 Walijibu na kumwambia, “Ulizaliwa katika dhambi kabisa, na wewe unatufundisha sisi?” Ndipo walipomfukuza kutoka katika sinagogi.
Odgovoré in rekó mu: Ves v grehih si se rodil, pa boš ti nas učil? In izženó ga ven.
35 Yesu alisikia kwamba wamemwondoa kwenye sinagogi. Alimpata na kumwambia, “Unamwamini Mwana wa Mtu?”
Jezus zasliši, da so ga izgnali ven; in ko ga najde, reče mu: Veruješ li v sina Božjega?
36 Alijibu na kusema, “Ni nani, Bwana, ili nami nipate kumwamini?”
On odgovorí in reče: Kdo je, gospod, da bom veroval va-nj?
37 Yesu akamwambia, “Umeshamuona, naye unayezungumza naye ndiye.”
Jezus mu pa reče: In videl si ga, in kteri s teboj govori, ta je.
38 Yule mtu akasema, “Bwana, Naamini.” Ndipo akamsujudia.
On pa reče: Verujem, gospod! In pokloni mu se.
39 Yesu akasema, “Kwa hukumu nimekuja katika Ulimwengu huu ili kwamba wale wasioona wapate kuona na wale wanaoona wawe vipofu.”
In Jezus reče: Jaz sem prišel na sodbo na ta svet, da kteri ne vidijo, spregledajo, in kteri vidijo, oslepé.
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye wakasikia maneno hayo na kumwuliza, “Na sisi pia ni vipofu?”
In slišali so to nekteri izmed Farizejev, kteri so bili ž njim, in rekó mu: Ali smo tudi mi slepi?
41 Yesu akawaambia, “Kama mngelikuwa vipofu, msingelikuwa na dhambi. Hata hivyo, sasa mnasema, 'Tunaona,' dhambi yenu inakaa.”
Reče jim Jezus: Ko bi bili slepi, ne bi imeli greha; sedaj pa pravite: Vidimo; za to greh vaš ostane.

< Yohana 9 >