< Yohana 8 >

1 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Yesu alienda mlima wa Mizeituni.
Et Jésus s’en alla à la montagne des Oliviers.
2 Mapema asubuhi akaja tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; akakaa na kuwafundisha.
Et au point du jour il vint encore au temple, et tout le peuple vint à lui; et s’étant assis, il les enseignait.
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha kuzini. Wakamweka katikati.
Et les scribes et les pharisiens lui amènent une femme surprise en adultère; et l’ayant placée devant lui,
4 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Ndipo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, mwanamke huyu amekamatwa katika uzinzi, katika kitendo kabisa.
ils lui disent: Maître, cette femme a été surprise sur le fait même, commettant adultère.
5 Sasa, katika sheria, Musa ametuamuru kuwaponda mawe watu kama hawa, unasemaje juu yake?
Or, dans la loi, Moïse nous a commandé de lapider de telles femmes: toi donc, que dis-tu?
6 Walisema haya ili kumtega ili kwamba wapate jambo la kumshitaki, lakini Yesu akainama chini akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
Or ils disaient cela pour l’éprouver, afin qu’ils aient de quoi l’accuser. Mais Jésus, s’étant baissé, écrivait avec le doigt sur la terre.
7 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Walipoendelea kumwuliza, alisimama na kuwaambia, “Yeye asiyekuwa na dhambi miongoni mwenu, awe wa kwanza kumponda mawe.”
Et comme ils continuaient à l’interroger, s’étant relevé, il leur dit: Que celui de vous qui est sans péché, jette le premier la pierre contre elle.
8 Akainama tena chini, akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
Et s’étant encore baissé, il écrivait sur la terre.
9 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Waliposikia hayo, waliondoka mmoja baada ya mwingine, kuanzia aliye mzee. Mwishowe Yesu aliachwa peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao.
Et eux, l’ayant entendu, sortirent un à un, en commençant depuis les plus anciens jusqu’aux derniers; et Jésus fut laissé seul avec la femme devant lui.
10 Yesu alisimama na kumwambia, “Mwanamke, waliokushitaki wako wapi? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
Et Jésus, s’étant relevé et ne voyant personne que la femme, lui dit: Femme, où sont-ils, ceux-là, tes accusateurs? Nul ne t’a-t-il condamnée?
11 Akasema, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda njia yako; kuanzia sasa na kuendelea usitende dhambi tena.”
Et elle dit: Nul, Seigneur. Et Jésus lui dit: Moi non plus, je ne te condamne pas; va, – dorénavant ne pèche plus.
12 Tena Yesu akazungumza na watu akisema, “Mimi ni nuru ya ulimwengu; yeye anifuataye hatatembea gizani bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Jésus donc leur parla encore, disant: Moi, je suis la lumière du monde; celui qui me suit ne marchera point dans les ténèbres, mais il aura la lumière de la vie.
13 Mafarisayo wakamwambia, “Unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako siyo wa kweli.”
Les pharisiens donc lui dirent: Tu rends témoignage de toi-même; ton témoignage n’est pas vrai.
14 Yesu alijibu akawaambia, “Hata kama nitajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli. Ninajua mahali nilikotoka na kule ninakoenda, lakini ninyi hamjui mahali ninapotoka au kule ninakoenda.
Jésus répondit et leur dit: Quoique moi je rende témoignage de moi-même, mon témoignage est vrai, car je sais d’où je suis venu et où je vais; mais vous, vous ne savez pas d’où je viens et où je vais.
15 Nyinyi mnahukumu kimwili; mimi simhukumu yeyote.
Vous, vous jugez selon la chair; moi, je ne juge personne.
16 Mimi hata nikihukumu, hukumu yangu ni kweli kwa sababu siko peke yangu, bali niko pamoja na baba aliyenituma.
Et si aussi moi, je juge, mon jugement est vrai, car je ne suis pas seul, mais moi et le Père qui m’a envoyé.
17 Ndiyo, na katika sheria yenu imeandikwa kwamba ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
Et il est écrit aussi dans votre loi, que le témoignage de deux hommes est vrai.
18 Mimi ndiye ninayejishuhudia, na Baba aliyenituma ananishuhudia.”
Moi, je rends témoignage de moi-même; et le Père qui m’a envoyé rend aussi témoignage de moi.
19 Wakamwambia, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu, “mimi hamnijui wala Baba yangu hammjui; mngelikuwa mnanijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
Ils lui dirent donc: Où est ton père? Jésus répondit: Vous ne connaissez ni moi, ni mon Père; si vous m’aviez connu, vous auriez connu aussi mon Père.
20 Alisema maneno haya akiwa karibu na hazina alipokuwa akifundisha hekaluni, na hakuna hata mmoja aliyemkamata kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Il dit ces paroles dans le trésor, enseignant dans le temple; et personne ne le prit, parce que son heure n’était pas encore venue.
21 Basi akawaambia tena, “Ninaenda zangu; mtanitafuta na mtakufa katika dhambi zenu. Kule niendako, hamuwezi kuja.”
[Jésus] leur dit donc encore: Moi, je m’en vais, et vous me chercherez; et vous mourrez dans votre péché: là où moi je vais, vous, vous ne pouvez venir.
22 Wayahudi wakasema, “Atajiua mwenyewe, yeye ambaye alisema, 'kule niendako hamuwezi kuja'?”
Les Juifs donc disaient: Se tuera-t-il, qu’il dise: Là où moi je vais, vous, vous ne pouvez venir?
23 Yesu akawaambia, “Mnatoka chini; mimi natoka juu. Ninyi ni wa Ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
Et il leur dit: Vous êtes d’en bas; moi, je suis d’en haut: vous êtes de ce monde; moi, je ne suis pas de ce monde.
24 Kwa hiyo, naliwaambieni kuwa mtakufa katika dhambi zenu. Vinginevyo muamini kuwa MIMI NDIYE, mtakufa katika dhambi zenu”.
Je vous ai donc dit que vous mourrez dans vos péchés; car si vous ne croyez pas que c’est moi, vous mourrez dans vos péchés.
25 Kwa hiyo wakamwambia, “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia, Yale niliyowaambia tangu mwanzo.
Ils lui disaient donc: Toi, qui es-tu? Et Jésus leur dit: Absolument ce qu’aussi je vous dis.
26 Ninayo mambo mengi ya kuzungumza na kuhukumu juu yenu. Hata hivyo, yeye aliyenituma ni wa kweli; na mambo niliyoyasikia kutoka kwake, mambo haya nayasema kwa Ulimwengu.”
J’ai beaucoup de choses à dire de vous et à juger; mais celui qui m’a envoyé est vrai, et les choses que j’ai entendues de lui, moi, je les dis au monde.
27 Hawakumuelewa kwamba alikuwa akiongea nao kuhusu Baba.
Ils ne connurent pas qu’il leur parlait du Père.
28 Yesu akasema, “Mtakapomwinua juu Mwana wa Mtu, ndipo mtakapojua kuwa MIMI NDIYE, na kwamba sifanyi lolote kwa nafsi yangu. Kama Baba alivyonifundisha, ninazungumza mambo haya.
Jésus donc leur dit: Quand vous aurez élevé le fils de l’homme, alors vous connaîtrez que c’est moi, et que je ne fais rien de moi-même, mais que, selon que le Père m’a enseigné, je dis ces choses.
29 Yeye aliyenituma yuko pamoja nami, na yeye hajaniacha peke yangu, kwani kila mara nafanya yale yanayompendeza.”
Et celui qui m’a envoyé est avec moi; il ne m’a pas laissé seul, parce que moi, je fais toujours les choses qui lui plaisent.
30 Wakati Yesu akisema mambo haya, wengi walimwamini.
Comme il disait ces choses, plusieurs crurent en lui.
31 Yesu akasema kwa wale Wayahudi waliomwamini, “Ikiwa mtakaa katika neno langu, ndipo mtakuwa wanafunzi wangu kweli,
Jésus donc dit aux Juifs qui avaient cru en lui: Si vous persévérez dans ma parole, vous êtes vraiment mes disciples;
32 nanyi mtaijua kweli, na kweli itawaweka huru.”
et vous connaîtrez la vérité, et la vérité vous affranchira.
33 Walimjibu, “Sisi ni uzao wa Ibrahimu na kamwe hatujawahi kwa chini ya utumwa wa yeyote; utasemaje, “Tutawekwa huru?”
Ils lui répondirent: Nous sommes la postérité d’Abraham, et jamais nous n’avons été dans la servitude de personne; comment dis-tu, toi: Vous serez rendus libres?
34 Yesu aliwajibu, “Amini, amini, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jésus leur répondit: En vérité, en vérité, je vous dis: Quiconque pratique le péché est esclave du péché.
35 Mtumwa hakai nyumbani wakati wote; mwana hudumu siku zote. (aiōn g165)
Or l’esclave ne demeure pas dans la maison pour toujours; le fils y demeure pour toujours. (aiōn g165)
36 Kwa hiyo, ikiwa Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kabisa.”
Si donc le Fils vous affranchit, vous serez réellement libres.
37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Ibrahimu; mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halina nafasi ndani yenu.
Je sais que vous êtes la postérité d’Abraham; mais vous cherchez à me faire mourir, parce que ma parole n’a pas d’entrée auprès de vous.
38 Ninasema mambo ambayo nimeyaona pamoja na Baba yangu, na ninyi vile vile mnafanya mambo ambayo mliyasikia kutoka kwa baba yenu.”
Moi, je dis ce que j’ai vu chez mon Père; vous aussi donc, vous faites les choses que vous avez entendues de la part de votre père.
39 Walijibu na kumwambia, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, Kama mngelikuwa watoto wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu.
Ils répondirent et lui dirent: Abraham est notre père. Jésus leur dit: Si vous étiez enfants d’Abraham, vous feriez les œuvres d’Abraham;
40 Hata sasa mnatafuta kuniua, mtu aliyewaambia ukweli kwamba nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.
mais maintenant vous cherchez à me faire mourir, moi, un homme qui vous ai dit la vérité que j’ai entendue de Dieu: Abraham n’a pas fait cela.
41 Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia, “Hatukuzaliwa katika uzinzi, tunaye Baba mmoja, Mungu.”
Vous, vous faites les œuvres de votre père. Ils lui dirent donc: Nous ne sommes pas nés de la fornication; nous avons un père, Dieu.
42 Yesu akawaambia, “Ikiwa Mungu ni Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nimetoka kwa Mungu; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye alinituma.
Jésus leur dit: Si Dieu était votre père, vous m’aimeriez, car moi je procède de Dieu et je viens de lui; car je ne suis pas venu de moi-même, mais c’est lui qui m’a envoyé.
43 Kwa nini hamyaelewi maneno yangu? Kwa sababu hamuwezi kuvumilia kuyasikia maneno yangu.
Pourquoi n’entendez-vous pas mon langage? Parce que vous ne pouvez pas entendre ma parole.
44 Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
Vous, vous avez pour père le diable, et vous voulez faire les convoitises de votre père. Lui a été meurtrier dès le commencement, et il n’a pas persévéré dans la vérité, car il n’y a pas de vérité en lui. Quand il profère le mensonge, il parle de son propre fonds, car il est menteur, et le père du mensonge.
45 Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
Mais moi, parce que je dis la vérité, vous ne me croyez pas.
46 Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
Qui d’entre vous me convainc de péché? Si je dis la vérité, vous, pourquoi ne me croyez-vous pas?
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
Celui qui est de Dieu entend les paroles de Dieu; c’est pourquoi vous, vous n’entendez pas, parce que vous n’êtes pas de Dieu.
48 Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
Les Juifs répondirent et lui dirent: Ne disons-nous pas bien que tu es un Samaritain, et que tu as un démon?
49 Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
Jésus répondit: Moi, je n’ai point un démon, mais j’honore mon Père, et vous, vous jetez du déshonneur sur moi.
50 Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
Mais pour moi, je ne cherche pas ma gloire; il y en a un qui cherche, et qui juge.
51 Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.” (aiōn g165)
En vérité, en vérité, je vous dis: Si quelqu’un garde ma parole, il ne verra point la mort, à jamais. (aiōn g165)
52 Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kuwa una pepo. Abrahamu na mabii walikufa; lakini unasema, 'Ikiwa mtu atalishika neno langu, hataonja mauti'. (aiōn g165)
Les Juifs donc lui dirent: Maintenant nous connaissons que tu as un démon: Abraham est mort, et les prophètes, et toi, tu dis: Si quelqu’un garde ma parole, il ne goûtera point la mort, à jamais. (aiōn g165)
53 Wewe si mkuu kuliko baba yetu Abrahamu aliyekufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Wewe wajifanya kuwa nani?”
Es-tu plus grand que notre père Abraham, qui est mort? et les prophètes sont morts. Qui te fais-tu toi-même?
54 Yesu akajibu, “Ikiwa nitajitukuza mwenyewe, utukufu wangu ni bure; ni Baba yangu anayenitukuza - yule mnayemsema kuwa ni Mungu wenu.
Jésus répondit: Si moi je me glorifie moi-même, ma gloire n’est rien; c’est mon Père qui me glorifie, lui de qui vous dites: Il est notre Dieu.
55 Ninyi hamjamjua yeye, lakini mimi namjua yeye. Ikiwa nitasema, 'simjui,' nitakuwa kama nyinyi, muongo. Hata hivyo, ninamjua na maneno yake nimeyashika.
Et vous ne le connaissez pas; mais moi, je le connais: et si je disais que je ne le connais pas, je serais menteur, semblable à vous; mais je le connais, et je garde sa parole.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia atakavyoiona siku yangu; aliiona na alifurahi.”
Abraham, votre père, a tressailli de joie de ce qu’il verrait mon jour; et il l’a vu, et s’est réjoui.
57 Wayahudi wakamwambia,”Haujafikisha umri wa miaka hamsini bado, nawe umemuona Ibrahimu?”
Les Juifs donc lui dirent: Tu n’as pas encore 50 ans, et tu as vu Abraham!
58 Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO.”
Jésus leur dit: En vérité, en vérité, je vous dis: Avant qu’Abraham fût, je suis.
59 Ndipo waliokota mawe wapate kumpiga, lakini Yesu alijificha na akatoka nje ya hekalu.
Ils prirent donc des pierres pour les jeter contre lui; mais Jésus se cacha et sortit du temple.

< Yohana 8 >