< Yohana 7 >

1 Na baada ya mambo haya Yesu alisafiri hivi katika Galilaya, kwa sababu hakupenda kwenda Uyahudi kwa sababu wayahudi walikuwa wakifanya mipango ya kumwua.
After these things, Jesus walked in Galilee, for He didn’t want to walk in Judea, because the Jews sought to kill Him.
2 Sasa sikukuu ya Wayahudi, sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu.
Now the Jews’ Feast of Tabernacles was near.
3 Ndipo ndugu zake walipomwambia, “Ondoka mahali hapa uende Uyahudi, ili kwamba wanafunzi wako vile vile wayaone matendo ufanyayo.
Therefore His brothers told Him, “Leave here and go to Judea, so that Your disciples will see the works that You are doing, too.
4 Hakuna afanyaye lolote kwa siri iwapo yeye mwenyewe anataka kujulikana wazi. Iwapo unafanya mambo haya, jionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”
Nobody does anything in secret while he seeks to be known openly. If You do these things, show Yourself to the world.”
5 Hata ndugu zake pia hawakumwamini.
For even His brothers didn’t believe in Him.
6 Ndipo Yesu alipowaambia, “Wakati wangu haujafika bado, lakini wakati wenu kila mara uko tayari.
Then Jesus told them, “My time hasn’t yet come, but your time is always right.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, bali unanichukia mimi kwa sababu ninaushuhudia kuwa matendo yake ni maovu.
The world can’t hate you, but it hates me because I testify that its works are evil.
8 Pandeni kwenda katika sikukuu; mimi siendi katika sikukuu hii kwa sababu muda wangu haujakamilika bado.”
Go up to this feast yourselves. I’m not going up to this feast, yet, for my time hasn’t yet fully come.”
9 Baada ya kusema mambo hayo kwao, alibaki Galilaya.
Having said these things to them, He stayed in Galilee.
10 Hata hivyo, ndugu zake walipokuwa wamekwenda katika sikukuu, ndipo naye alienda, siyo kwa wazi bali kwa siri.
When His brothers had gone up to the feast, however, Jesus also went up, not publicly, but in secret.
11 Wayahudi walikuwa wakimtafuta katika sikukuu na kusema, “Yuko wapi?”
The Jews were looking for Him at the feast, and saying, “Where is He?”
12 Kulikuwa na majadiliano mengi miongoni mwa makutano juu yake. Wengine walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “Hapana, huwapotosha makutano.”
There was much complaining among the people about Him. Some said, “He is good,” but others said, “No, He deceives the people.”
13 Hata hivyo hakuna aliyezungumza wazi juu yake kwa kuwaogopa Wayahudi.
No one spoke openly of Him for fear of the Jews.
14 Wakati sikukuu ilipofika katikati, Yesu alipanda kwenda Hekaluni na kuanza kufundisha.
About the middle of the feast, Jesus went up into the temple and began to teach.
15 Wayahudi walikuwa wakishangaa na kusema, “Kwa jinsi gani mtu huyu anajua mambo mengi? Hajasoma kamwe.”
The Jews marveled, saying, “How does this man know letters, having never been educated?”
16 Yesu akawajibu na kuwaambia, “Mafundisho yangu siyo yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Jesus answered, “My teaching isn’t mine, but His who sent me.
17 Iwapo yeyote atapenda kufanya mapenzi yake yeye, atajua kuhusu mafundisho haya, kama yanatoka kwa Mungu, au kama ninazungumza kutoka kwangu mwenyewe.
Anyone who wants to do His will shall know if the teaching is from God or if I speak on my own.
18 Kila anayezungumza yatokayo kwake mwenywe hutafuta utukufu wake, bali kila atafutaye utukufu wake yeye aliyemtuma, mtu huyo ni wa kweli, na ndani yake hakuna kutotenda haki.
The one who speaks on his own seeks his own glory; but He who seeks the glory of the One who sent Him is true, and no unrighteousness is in Him.
19 Musa hakuwapa nyinyi sheria? Lakini hakuna hata mmoja kati yenu atendaye sheria. Kwa nini mnataka kuniua?
Didn’t Moses give you the Law, yet none of you keeps the Law? Why are you trying to kill me?”
20 Makutano wakajibu, “Una pepo. Nani anataka kukuua?”
The people answered, “You have a demon. Who is trying to kill You?”
21 Yesu akajibu na akawaambia, “Nimetenda kazi moja, nanyi nyote mmeshangazwa kwa sababu yake.
Jesus answered, “I did one work, and you all marvel.
22 Musa aliwapa tohara (siyo kwamba inatoka kwa Musa, bali ile inatoka kwa mababa), na katika Sabato mnamtahili mtu.
Moses gave you circumcision (not that it’s from Moses, but from the forefathers), and you circumcise a boy on the Sabbath.
23 Iwapo mtu atapokea tohara katika siku ya Sabato ili kwamba sheria ya Musa isivunjwe, kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa katika Sabato?
If a boy gets circumcised on the Sabbath, so that the Law of Moses should not be broken, are you angry with me because I made a man completely well on the Sabbath?
24 Msihukumu kulingana na mwonekano, bali hukumuni kwa haki.
Don’t judge by appearance, but judge with righteous judgment.”
25 Baadhi yao kutoka Yerusalemu wakasema, “Siye huyu wanayemtafuta kumwua?
Some of the people of Jerusalem said, “Isn’t this the man they are trying to kill?
26 Na tazama, anaongea wazi wazi, na hawasemi chochote juu yake. Haiwezi ikawa kwamba viongozi wanajua kweli kuwa huyu ni Kristo, inaweza kuwa?
Look! He is speaking boldly, and they say nothing to Him. The rulers haven’t really concluded that this is the Christ, have they?
27 Tunajua huyu mtu anatokea wapi. Kristo atakapokuja, hata hivyo, hakuna atakayejua wapi anakotoka.”
Still, we know where this man is from, but when the Christ comes, no one will know where He is from.”
28 Yesu alikuwa akipaza sauti yake hekaluni, akifundisha na kusema, “Ninyi nyote mnanijua mimi na mnajua nitokako. Sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye aliyenituma ni wa kweli, na hamumjui yeye.
Then Jesus cried out, as He taught in the temple, “You know me, and you know where I’m from. I haven’t come of my own accord, but He who sent me is true, who you don’t know.
29 Ninamjua yeye kwa sababu nimetoka kwake na alinituma.”
I know Him, because I am from Him, and He sent me.”
30 Walikuwa wanajaribu kumkamata, lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono wake juu yake kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Because of this, they were seeking to seize Him, but no one laid hands on Him, because His time had not yet come.
31 Hata hivyo, wengi katika makutano walimwamini. Walisema, “Kristo atakapokuja, atafanya ishara nyingi kuliko alizofanya mtu huyu?”
Many of the people believed in Him, saying, “When the Christ comes, will He do more signs than this man has done?”
32 Mafarisayo waliwasikia makutano wakinong'onezana mambo haya kuhusu Yesu, na wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakatuma maafisa ili kumkamata.
The Pharisees heard the crowd murmuring these things about Jesus, and the Pharisees and the chief priests sent officers to seize Him.
33 Ndipo Yesu aliposema, “Bado kuna muda kitambo niko pamoja nanyi, na baadaye nitakwenda kwake yeye aliyenituma.
Then Jesus told them, “I will be with you a little while longer, and then I am going to Him who sent me.
34 Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako, hamtaweza kuja.”
You will look for me, and not find me, and where I am, you can’t come.”
35 Kwa hiyo Wayahudi wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi kwamba tusiweze kumuona? Ataenda kwa Waliotawanyika kati ya Wayunani na kuwafundisha Wayunani?
Then the Jews said among themselves, “Where does He intend to go that we won’t be able to find Him? He doesn’t intend to go to the dispersion among the Greeks and teach the Greeks, does He?
36 Ni neno gani hili alilolisema, 'Mtanitafuta wala hamtaniona; kule niendako hamtamweza kuja'?”
What does He mean by saying, ‘You will look for me, and not find me, and where I am, you can’t come’?”
37 Sasa katika siku ya mwisho, siku kubwa ya sikukuu, Yesu alisimama akapaza sauti, akisema, “Ikiwa yeyote ana kiu, na aje kwangu anywe.
On the last and greatest day of the feast, Jesus stood and declared loudly, “If anyone is thirsty, let that person come to me and drink.
38 Yeye aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyosema, kutoka ndani yake itatiririka mito ya maji ya uzima.”
Rivers of living water will flow from within whoever believes in me, as the Scripture has said.”
39 Lakini aliyasema haya kuhusu Roho, ambaye wao wamwaminio watampokea; Roho alikuwa bado hajatolewa kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.
He said this about the Spirit, who those believing in Him would receive. The Holy Spirit wasn’t yet given, because Jesus wasn’t yet glorified.
40 Baadhi ya makutano, waliposikia maneno haya, walisema, “Kweli huyu ni nabii.”
When they heard these words, many in the crowd were saying, “This is really the prophet.”
41 Wengine walisema, “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine walisema, “nini, Kristo aweza kutoka Galilaya?
Others were saying, “This is the Christ,” but some were saying, “Surely the Christ isn’t going to come from Galilee, is He?
42 Maandiko hayajasema kuwa Kristo atatokea katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa?
Hasn’t the Scripture said that the Christ comes from the seed of David and from the town of Bethlehem, where David was?”
43 Hivyo, pale ukainuka mgawanyiko katikati ya makutano kwa ajili yake.
So there was a division among the crowd because of Jesus.
44 Wengine kati yao wangelimkamata, lakini hakuna aliyenyoosha mikono yake juu yake.
Some of them wanted to seize Him, but no one laid hands on Him.
45 Ndipo wale maofisa wakarudi kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, nao wakawaambia, “Kwa nini hamjamleta?”
When the officers went back to the chief priests and Pharisees, they asked them, “Why didn’t you bring Him in?”
46 Maofisa wakajibu, “Hakuna mtu aliyewahi kuzungumza kama huyu kabla.”
The officers answered, “No man ever spoke like this man!”
47 Ndipo Mafarisayo walipowajibu, “Na nyinyi pia mmepotoshwa?
Then the Pharisees answered, “You haven’t been deceived, too, have you?
48 Kuna yeyote kati ya watawala anayemwamini, au yeyote wa Mafarisayo?
Have any of the rulers or Pharisees believed in Him?
49 Bali hawa makutano wasiojua sheria - wamelaaniwa.”
But this accursed crowd doesn’t know the Law.”
50 Nikodemo akawaambia (yeye aliyemwendea Yesu zamani, akiwa mmoja wa Mafarisayo),
Nicodemus (who came to Jesus before, being one of them) asked them,
51 “Je sheria yetu inamhukumu mtu isipokuwa amesikilizwa kwanza na kujua anachokifanya?”
“Does our Law permit us to judge a man before hearing him and finding out what he is doing?”
52 Walijibu na kumwambia, “Na wewe pia unatokea Galilaya? Tafuta na uone kwamba hakuna nabii aliyetokea Galilaya.”
They answered him, “You aren’t from Galilee, too, are you? Search and you will see that no prophet comes out of Galilee.”
53 (Zingatia: Baadhi ya maneno ya Yohana 7: 53 - 8: 11 hayamo katika nakala bora za kale). Kisha kila mtu alienda nyumbani kwake.
Then everyone went home,

< Yohana 7 >