< Yohana 2 >

1 Baada ya siku tatu, kulikuwa na arusi huko Kana ya Galilaya na mama yake Yesu alikuwa huko.
Et le troisième jour, il y eut une noce à Cana de Galilée, et la mère de Jésus était là.
2 Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa katika arusi.
Et Jésus fut aussi convié à la noce, ainsi que ses disciples.
3 Wakati walipoishiwa na divai, mama yake Yesu akamwambia, “Hawana divai.”
Et le vin étant venu à manquer, la mère de Jésus lui dit: Ils n’ont pas de vin.
4 Yesu akajibu, “Mwanamke hiyo inanihusu nini mimi? Muda wangu mimi bado haujatimia.”
Jésus lui dit: Qu’y a-t-il entre moi et toi, femme? Mon heure n’est pas encore venue.
5 Mama yake akawambia watumishi, “Chochote atakachowambia fanyeni.”
Sa mère dit aux serviteurs: Faites tout ce qu’il vous dira.
6 Basi kulikuwa na mitungi sita ya mawe pale iliyowekwa kwa ajili ya kunawa katika sikukuu za Wayahudi, kila moja lilikuwa na ujazo wa nzio mbili tatu.
Or il y avait là six vaisseaux de pierre, pour tenir de l’eau, placés là selon [l’usage de] la purification des Juifs, pouvant recevoir chacun deux ou trois mesures.
7 Yesu akawambia, “Ijazeni maji mitungi ya mawe.” Wakajaza hadi juu.
Jésus leur dit: Emplissez d’eau les vaisseaux. Et ils les emplirent jusqu’au haut.
8 Kisha akawambia wale watumishi, “Chukueni kiasi sasa na mpeleke kwa muhudumu mkuu wa meza.” Wakafanya kama walivyoagizwa.
Et il leur dit: Puisez maintenant, et portez-en au maître d’hôtel. Et ils lui en portèrent.
9 Mhudumu mkuu aliyaonja yale maji yaliyokuwa yamebadilika na kuwa divai, ila hakujua yalikotoka (lakini watumishi waliochota maji walijua yalikotoka). Kisha akamwita bwana harusi na
Mais lorsque le maître d’hôtel eut goûté l’eau qui était devenue du vin, et qu’il ne savait point d’où celui-ci venait (mais les serviteurs qui avaient puisé l’eau le savaient), le maître d’hôtel appelle l’époux,
10 kumwambia, “Kila mmoja huanza kuwahudumia watu divai nzuri na wakiishalewa huwapa divai isiyo nzuri. Lakini wewe umeitunza divai nzuri hadi sasa”
et lui dit: Tout homme sert le bon vin le premier, et puis le moindre, après qu’on a bien bu; toi, tu as gardé le bon vin jusqu’à maintenant.
11 Muujiza huu wa Kana ya Galilaya, ulikuwa ndio mwanzo wa ishara za miujiza aliyoifanya Yesu, akifunua utukufu wake, hivyo wanafunzi wake wakamwamini.
Jésus fit ce commencement de [ses] miracles à Cana de Galilée, et il manifesta sa gloire; et ses disciples crurent en lui.
12 Baada ya hii, Yesu, mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake walienda katika mji wa Kapernaum na wakaa huko kwa siku chache.
Après cela, il descendit à Capernaüm, lui et sa mère et ses frères et ses disciples; et ils y demeurèrent peu de jours.
13 Basi Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia, hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
Et la Pâque des Juifs était proche, et Jésus monta à Jérusalem.
14 Akawakuta wauzaji wa ng'ombe, kondoo, na njiwa ndani ya Hekalu. Pia na wabadilisha fedha walikuwa wameketi ndani ya Hekalu.
Et il trouva dans le temple les vendeurs de bœufs et de brebis et de colombes, et les changeurs qui y étaient assis.
15 Yesu akatengeneza mjeledi wenye vifundo, akawatoa wote walikuwemo katika hekalu, ikijumuisha ng'ombe na kondoo. Akamwaga fedha za wabadili fedha na kuzipindua meza zao.
Et ayant fait un fouet de cordes, il les chassa tous hors du temple, et les brebis et les bœufs; et il répandit la monnaie des changeurs et renversa les tables.
16 Kwa wauzaji wa njiwa akawambia, “Toeni vitu hivi mbali na mahali hapa, acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa soko.”
Et il dit à ceux qui vendaient les colombes: Ôtez ces choses d’ici; ne faites pas de la maison de mon Père une maison de trafic.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa ilikuwa imeandikwa, “Wivu wa nyumba yako utanila.”
[Et] ses disciples se souvinrent qu’il est écrit: « Le zèle de ta maison me dévore ».
18 Wakuu wa Kiyahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara ipi utakayoionyesha kwa sababu unayafanya mambo haya?”
Les Juifs donc répondirent et lui dirent: Quel miracle nous montres-tu, que tu fasses ces choses?
19 Yesu akawajibu, libomoeni Hekalu hili nami nitalijenga baada ya siku tatu.”
Jésus répondit et leur dit: Détruisez ce temple, et en trois jours je le relèverai.
20 Kisha wakuu wa Wayahudi wakasema, “Iligharimu miaka arobaini na sita kujenga hekalu hili nawe unasema utalijenga kwa siku tatu?”
Les Juifs donc dirent: On a été 46 ans à bâtir ce temple, et toi, tu le relèveras en trois jours!
21 Ingawa, yeye aliongea hekalu akimaanisha mwili wake.
Mais lui parlait du temple de son corps.
22 Hivyo baadaye baada ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka kuwa alisema hivyo, wakaamini maandiko na kauli hii ambayo Yesu alikuwa amekwisha kuisema.
Lors donc qu’il fut ressuscité d’entre les morts, ses disciples se souvinrent qu’il avait dit cela; et ils crurent à l’écriture, et à la parole que Jésus avait dite.
23 Basi alipokuwa Yerusalemu wakati wa Pasaka, wakati wa sikukuu watu wengi waliamini jina lake, walipoona ishara ya miujiza aliyoifanya.
Et comme il était à Jérusalem, à la Pâque, pendant la fête, plusieurs crurent en son nom, contemplant les miracles qu’il faisait.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
Mais Jésus lui-même ne se fiait pas à eux, parce qu’il connaissait tous [les hommes],
25 Hakuhitaji mtu yeyote kumwambia kuhusu walivyo wanadamu kwa sababu alijua kilichokuwamo ndani yao.
et qu’il n’avait pas besoin que quelqu’un rende témoignage au sujet de l’homme; car lui-même connaissait ce qui était dans l’homme.

< Yohana 2 >