< Joeli 3 >

1 Tazama, katika siku hizo na wakati huo, nitakaporudi mateka wa Yuda na Yerusalemu,
For, behold, in those days, and in that time, when I shall bring back the captivity of Judah and Jerusalem,
2 Nami nitakusanya mataifa yote, na kuwaleta mpaka bonde la Yehoshafati. Nitawahukumu huko, kwa sababu ya watu wangu na warithi wangu Israeli, ambao waliwatawanya kati ya mataifa, na kwa sababu waligawanya nchi yangu.
I will gather all nations, and will bring them down into the valley of Jehoshaphat; and I will enter into judgment with them there for My people and for My heritage Israel, whom they have scattered among the nations, and divided My land.
3 Wamepiga kura kwa ajili ya watu wangu, walinunua kijana kwa ajili ya kahaba, kuuza msichana kwa divai ili waweze kunywa.
And they have cast lots for My people; and have given a boy for an harlot, and sold a girl for wine, and have drunk.
4 Sasa, kwa nini unanikasirikia, Tiro, Sidoni na mikoa yote ya Wafilisti? Je! mutanirudishia malipo? Hata kama mutanilipa, mara moja nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe.
And also what are ye to Me, O Tyre, and Zidon, and all the regions of Philistia? will ye render retribution on My behalf? and if ye render retribution on My behalf, swiftly, speedily will I return your retribution upon your own head.
5 Kwa maana mumechukua fedha zangu na dhahabu zangu, nanyi mukachukua hazina zangu za thamani na kuzileta katika hekalu zenu.
Forasmuch as ye have taken My silver and My gold, and have carried into your temples My goodly treasures;
6 Mumewauza watu wa Yuda na Yerusalemu kwa Wayunani, ili kuwaondoa mbali na maeneo yao.
the children also of Judah and the children of Jerusalem have ye sold unto the sons of Jevanim, that ye might remove them far from their border;
7 Tazama, nitawaamsha, watoke mahali ambako muliwauza, na nitawarudishia malipo juu ya vichwa vyenu wenyewe.
behold, I will stir them up out of the place whither ye have sold them, and will return your retribution upon your own head;
8 Nitawauza wana wako na binti zako, kwa mkono wa watu wa Yuda. Wao watawauza Sheba, kwa taifa mbali. Kwa maana Bwana amesema.
and I will sell your sons and your daughters into the hand of the children of Judah, and they shall sell them to the men of Sheba, to a nation far off; for the LORD hath spoken.
9 Tangaza hii kati ya mataifa, 'Jitayarisheni wenyewe kwa ajili ya vita, waamsheni mashujaa, waacheni wakaribie, mashujaa wote wa vita wapande juu.
Proclaim ye this among the nations, prepare war; stir up the mighty men; let all the men of war draw near, let them come up.
10 Yafueni majembe yenu kuwa panga na visu vyenu vya kuchongea kuwa mikuki. Basi wadhaifu waseme, 'Nina nguvu.'
Beat your plowshares into swords, and your pruning-hooks into spears; let the weak say: 'I am strong.'
11 Haraka na mje, mataifa yote ya karibu, jikusanyeni pamoja huko. Ee Bwana, washushe mashujaa wako.
Haste ye, and come, all ye nations round about, and gather yourselves together; thither cause Thy mighty ones to come down, O LORD!
12 Naam, mataifa yajihimize yenyewe kuja hadi bonde la Yehoshafati. Kwa maana nitakaa huko kuhukumu mataifa yote ya jirani.
Let the nations be stirred up, and come up to the valley of Jehoshaphat; for there will I sit to judge all the nations round about.
13 Wekeni katiki mundu, kwa maana mavuno yameiva. Njoo, muponde zabibu, kwa ajiri pipa la divai limejaa. Vipuri vilivyofurika, kwa sababu uovu wao ni mkubwa sana.
Put ye in the sickle, for the harvest is ripe; come, tread ye, for the winepress is full, the vats overflow; for their wickedness is great.
14 Kuna mshtuko, mshtuko katika bonde la Hukumu. Kwa maana siku ya Bwana i karibu katika bonde la hukumu.
Multitudes, multitudes in the valley of decision! For the day of the LORD is near in the valley of decision.
15 Jua na mwezi vinakuwa giza, nyota zimeacha kuangaza.
The sun and the moon are become black, and the stars withdraw their shining.
16 Bwana ataunguruma kutoka Sayuni, na kuinua sauti yake kutoka Yerusalemu. Mbingu na nchi zitatikisika, lakini Bwana atakuwa makao kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa wana wa Israeli.
And the LORD shall roar from Zion, and utter His voice from Jerusalem, and the heavens and the earth shall shake; but the LORD will be a refuge unto His people, and a stronghold to the children of Israel.
17 Kwa hiyo mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, anayeishi Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Kisha Yerusalemu itakuwa takatifu, na hakuna jeshi litaklozunguka tena.
So shall ye know that I am the LORD your God, dwelling in Zion My holy mountain; then shall Jerusalem be holy, and there shall no strangers pass through her any more.
18 Katika siku hiyo, milima itatayarisha divai nzuri, milima itatiririsha maziwa, miito yote ya Yuda itapita katikati ya maji, na chemchemi zitakuja kutoka nyumba ya Bwana na maji ya bonde la Shitimu.
And it shall come to pass in that day, that the mountains shall drop down sweet wine, and the hills shall flow with milk, and all the brooks of Judah shall flow with waters; and a fountain shall come forth of the house of the LORD, and shall water the valley of Shittim.
19 Misri itakuwa ukiwa, na Edomu itakuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vurugu iliyofanyika kwa watu wa Yuda, kwa sababu walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.
Egypt shall be a desolation, and Edom shall be a desolate wilderness, for the violence against the children of Judah, because they have shed innocent blood in their land.
20 Lakini Yuda utakua mwenyeji milele, na Yerusalemu itakuwa kizazi hata kizazi.
But Judah shall be inhabited for ever, and Jerusalem from generation to generation.
21 Nitawalipizia damu yao, ambayo sijajilipizia kisasi, kwa maana Bwana anaishi Sayuni.
And I will hold as innocent their blood that I have not held as innocent; and the LORD dwelleth in Zion.

< Joeli 3 >