< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
And he answered Job and he said.
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Truly I know that thus and what? will he be justified a person with God.
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
If someone desires to conduct a case with him not he will answer him one [time] from a thousand.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Wise of heart and strong of power who? has he shown stubbornness to him and he has remained unharmed.
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
The [one who] removes mountains and not they know [the one] who he overturns them in anger his.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
The [one who] shakes [the] earth from place its and pillars its they tremble!
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
The [one who] speaks to the sun and not it shines and behind [the] stars he puts a seal.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
[one who] stretches out [the] heavens To only him and [one who] treads on [the] high places of [the] sea.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
[one who] makes [the] Bear Orion and Pleiades and [the] chambers of [the] south.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
[one who] does Great [things] until there not [is] inquiry and wonders until there not [is] number.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
There! he will pass by at me and not I will see [him] and he may pass on and not I will perceive him.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
There! he will snatch away who? will he turn back him who? will he say to him what? are you doing.
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
God not he will turn back anger his (under him *Qk) they lay prostrate [the] helpers of Rahab.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Indeed? for I I will answer him I will choose words my with him.
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
[I] who Though I am righteous not I will answer to judge my I will seek favor.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
If I called and he answered me not I believe that he gave ear to voice my.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
[he] who With a storm he crushes me and he increases wounds my without cause.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Not he permits me to bring back breath my for he surfeits me bitter things.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
If to power a strong [one] there! and if to justice who? will he summon me.
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Though I am righteous own mouth my it will condemn as guilty me [am] blameless I and it declared guilty me.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
[am] blameless I not I know self my I reject life my.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
[is] one It there-fore I say [the] blameless and [the] wicked he [is] bringing to an end.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
If a scourge it kills suddenly [the] despair of innocent [ones] he mocks.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
A land - it has been given in [the] hand of a wicked [person] [the] face of judges its he covers if not then who? [is] it.
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
And days my they have been swift more than a runner they have fled not they have seen good.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
They have passed on with ships of reed like an eagle [which] it rushes on food.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
If to say I I will forget complaint my I will let loose face my and I will be cheerful.
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
I dread all pains my I know that not you will acquit me.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
I I will be guilty why? this vanity will I labor.
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
If I washed myself (in water of *QK) snow and I cleansed with potash hands my.
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Then in pit you will dip me and they will abhor me own clothes my.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
For not [he is] a human like me I will answer him we will come together in judgment.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Not there between us [is] an arbiter he may put hand his on [the] two of us.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Let him remove from on me rod his and dread his may not it terrify me.
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
I will speak and not I will fear him for not [am] thus I with myself.

< Ayubu 9 >