< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
And Job, responding, said:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Truly, I know that it is so, and that man cannot be justified compared with God.
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
If he chooses to contend with him, he is not able to respond to him once out of a thousand times.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
He is understanding in heart and mighty in strength; who has resisted him and yet had peace?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
He has moved mountains, and those whom he overthrew in his fury did not know it.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
He shakes the earth out of its place and its pillars tremble.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
He commands the sun and it does not rise, and he closes the stars as if under a seal.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
He alone extends the heavens, and he walks upon the waves of the sea.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
He fashions Arcturus, and Orion, and Hyades, and the interior of the south.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
He accomplishes great and incomprehensible and miraculous things, which cannot be numbered.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
If he approaches me, I will not see him; if he departs, I will not understand.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
If he suddenly should question, who will answer him? Or who can say, “Why did you do so?”
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
God, whose wrath no one is able to resist, and under whom they bend who carry the world,
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
what am I then, that I should answer him and exchange words with him?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
And if I now have any justice, I will not respond, but will beseech my judge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
And if he should listen to me when I call, I would not believe that he had heard my voice.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
For he will crush me in a whirlwind and multiply my wounds, even without cause.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
He does not permit my spirit to rest, and he fills me with bitterness.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
If strength is sought, he is most strong; if equity in judgment, no one would dare to give testimony for me.
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
If I wanted to justify myself, my own mouth will condemn me; if I would reveal my innocence, he would prove me depraved.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
And if I now became simple, my soul would be ignorant even of this, and my life would weary me.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
There is one thing that I have said: both the innocent and the impious he consumes.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
If he scourges, let him kill all at once, and not laugh at the punishment of the innocent.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
Since the earth has been given into the hand of the impious, he covers the face of its judges; for if it is not him, then who is it?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
My days have been swifter than a messenger; they have fled and have not seen goodness.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
They have passed by like ships carrying fruits, just like an eagle flying to food.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
If I say: “By no means will I speak this way.” I change my face and I am tortured with sorrow.
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
I have dreaded all my works, knowing that you did not spare the offender.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Yet, if I am also just as impious, why have I labored in vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
If I had been washed with snow-like waters, and my hands were shining like the cleanest thing,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
yet you would plunge me in filth, and my own garments would abhor me.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
For even I would not answer a man who were like myself, nor one who could be heard with me equally in judgment.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
There is no one who could both prevail in argument and in placing his hand between the two.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Let him take his staff away from me, and let not the fear of him terrify me.
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
I will speak and I will not fear him, for in fearfulness I am not able to respond.

< Ayubu 9 >