< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Then Baldad the Sauchite answered, and said,
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
How long will you speak these things, [how long shall] the breath of your mouth [be] abundant in words?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Will the Lord be unjust when he judges; or will he that has made all things pervert justice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
If your sons have sinned before him, he has cast them away because of their transgression.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
But be you early in prayer to the Lord Almighty.
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
If you are pure and true, he will listen to your supplication, and will restore to you the habitation of righteousness.
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
Though then your beginning should be small, yet your end should be unspeakably great.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
For ask of the former generation, and search diligently amongst the race of [our] fathers:
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(for we are of yesterday, and know nothing; for our life upon the earth is a shadow: )
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
shall not these teach you, and report [to you], and bring out words from [their] heart?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Does the rush flourish without water, or shall the flag grow up without moisture?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
When it is yet on the root, and [though] it has not been cut down, does not any herb wither before it has received moisture?
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Thus then shall be the end of all that forget the Lord: for the hope of the ungodly shall perish.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
For his house shall be without inhabitants, and his tent shall prove a spider's web.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
If he should prop up his house, it shall not stand: and when he has taken hold of it, it shall not remain.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
For it is moist under the sun, and his branch shall come forth out of his dung-heap.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
He lies down upon a gathering of stones, and shall live in the mist of flints.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
If [God] should destroy [him], his place shall deny him. Hast you not seen such things,
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
that such is the overthrow of the ungodly? and out of the earth another shall grow.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
For the Lord will by no means reject the harmless man; but he will not receive any gift of the ungodly.
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
But he will fill with laughter the mouth of the sincere, and their lips with thanksgiving.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
But their adversaries shall clothe themselves with shame; and the habitation of the ungodly shall perish.

< Ayubu 8 >