< Ayubu 7 >

1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
"Isn't a man forced to labor on earth? Aren't his days like the days of a hired hand?
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
As a servant who earnestly desires the shadow, as a hireling who looks for his wages,
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
so am I made to possess months of misery, wearisome nights are appointed to me.
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
When I lie down, I say, 'When shall I arise, and the night be gone?' I toss and turn until the dawning of the day.
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
My flesh is clothed with worms and clods of dust. My skin closes up, and breaks out afresh.
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
My days are swifter than a weaver's shuttle, and are spent without hope.
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
Oh remember that my life is a breath. My eye shall no more see good.
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
The eye of him who sees me shall see me no more. Your eyes shall be on me, but I shall not be.
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol h7585)
As the cloud is consumed and vanishes away, so he who goes down to Sheol shall come up no more. (Sheol h7585)
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
He shall return no more to his house, neither shall his place know him any more.
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
"Therefore I will not keep silent. I will speak in the anguish of my spirit. I will complain in the bitterness of my soul.
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
Am I a sea, or a sea monster, that you put a guard over me?
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
When I say, 'My bed shall comfort me. My couch shall ease my complaint;'
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
then you scare me with dreams, and terrify me through visions:
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
so that my soul chooses strangling, death rather than my bones.
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
I loathe my life. I do not want to live forever. Leave me alone, for my days are but a breath.
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
What is man, that you should magnify him, that you should set your mind on him,
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
that you should visit him every morning, and test him every moment?
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
How long will you not look away from me, nor leave me alone until I swallow down my spittle?
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
If I have sinned, what do I do to you, you watcher of men? Why have you set me as a mark for you, so that I am a burden to myself?
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
Why do you not pardon my disobedience, and take away my iniquity? For now shall I lie down in the dust. You will seek me diligently, but I shall not be."

< Ayubu 7 >