< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Entonces Job respondió:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
¡Oh, si se pesara mi angustia, y se pusiera igualmente en balanza juntamente con mi ruina!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
¡Pesarían ahora más que la arena del mar! Por eso mis palabras fueron precipitadas,
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
porque en mí están clavadas las flechas de ʼEL-Shadday. Mi espíritu sorbe su veneno, y terrores de ʼElohim me combaten.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
¿Rebuzca el asno montés junto a la hierba? ¿Muge el buey junto a su pasto?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
¿Se comerá lo insípido sin sal? ¿Hay sabor en la clara del huevo?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
Las cosas que mi alma rehusaba tocar son ahora mi alimento nauseabundo.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
¡Quién me diera obtener mi petición, y que ʼElohim me otorgue lo que tanto anhelo!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
¡Que ʼElohim se digne aplastarme, que suelte su mano y acabe conmigo!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Eso sería mi consuelo, y aun en medio de mi dolor que no da tregua, saltaría de gozo, porque no negué las Palabras del Santo.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
¿Cuál es mi fuerza para seguir esperando? ¿Cuál es mi propósito para que tenga aún paciencia?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
¿Es mi fortaleza como la de las piedras, o mi cuerpo es de bronce?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
¿Puedo sostenerme sobre nada? ¿No fue todo auxilio alejado de mí?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
Para el hombre desconsolado debe haber bondad de su amigo, a fin de que no abandone el temor a ʼEL-Shadday.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
Mis hermanos me traicionaron como un torrente. Pasan como corrientes impetuosas
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
que van turbias a causa del deshielo, y la nieve que se deshace en ellas.
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
En el tiempo del calor se desvanecen. Al calentarse desaparecen, se extinguen de su lugar.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
Se apartan de la senda de su rumbo, van menguando y se pierden.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
Las caravanas de Temán fijan su mirada en ellas, los viajeros de Sabá tienen su esperanza en ellas,
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
pero son avergonzados en su esperanza, pues llegan hasta ellas y quedan defraudados.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
En verdad ustedes son ahora como ellos. Ven un terror y temen.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
¿Yo les dije: Tráiganme algo? ¿O: Paguen de su hacienda por mí?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
¿O: Líbrenme de la mano del enemigo? ¿O: Rescátenme del poder del opresor?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Instrúyeme y me callaré. Hazme entender en qué erré.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
¡Cuán dolorosas son las palabras honestas! ¿Pero qué prueba su reprensión?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
¿Piensan ustedes censurar palabras y los dichos de un desesperado que son como el viento?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Ustedes aun echan suertes sobre los huérfanos y regatean con su amigo.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Ahora pues, dígnense mirarme y opinen si miento delante de ustedes.
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Les ruego que desistan. Que no haya iniquidad. Sí, que mi justicia aún permanezca.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
¿Hay iniquidad en mi lengua? ¿Mi paladar no distingue lo destructivo?

< Ayubu 6 >