< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered,
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
"Oh that my anguish were weighed, and all my calamity laid in the balances.
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now it would be heavier than the sand of the seas, therefore have my words been rash.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For the arrows of Shaddai are within me. My spirit drinks up their poison. The terrors of God set themselves in array against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Does the wild donkey bray when he has grass? Or does the ox low over his fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Can that which has no flavor be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
My soul refuses to touch them. They are as loathsome food to me.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
"Oh that I might have my request, that God would grant the thing that I long for,
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
even that it would please God to crush me; that he would let loose his hand, and cut me off.
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Be it still my consolation, yes, let me exult in pain that doesn't spare, that I have not denied the words of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What is my strength, that I should wait? What is my end, that I should be patient?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength the strength of stones? Or is my flesh of bronze?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Isn't it that I have no help in me, That wisdom is driven quite from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
"To the despairing, kindness should be shown from his friend; even to him who forsakes the fear of Shaddai.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
My brothers have dealt deceitfully as a brook, as the channel of brooks that pass away;
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Which are black by reason of the ice, in which the snow hides itself.
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
In the dry season, they vanish. When it is hot, they are consumed out of their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
The caravans that travel beside them turn aside. They go up into the waste, and perish.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The caravans of Tema looked. The companies of Sheba waited for them.
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They were distressed because they were confident. They came there, and were confounded.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For now you are nothing. You see a terror, and are afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Did I say, 'Give to me?' or, 'Offer a present for me from your substance?'
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
or, 'Deliver me from the adversary's hand?' or, 'Redeem me from the hand of the oppressors?'
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
"Teach me, and I will hold my peace. Cause me to understand wherein I have erred.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How forcible are words of uprightness. But your reproof, what does it reprove?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Do you intend to reprove words, seeing that the speeches of one who is desperate are as wind?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Yes, you would even cast lots for the fatherless, and make merchandise of your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Now therefore be pleased to look at me, for surely I shall not lie to your face.
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Please return. Let there be no injustice. Yes, return again. My cause is righteous.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there injustice on my tongue? Can't my taste discern mischievous things?

< Ayubu 6 >