< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
Oh that my vexation were but weighed, and my calamity laid in the balances altogether!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now it would be heavier than the sand of the seas; therefore are my words broken.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty are within me, the poison whereof my spirit drinketh up; the terrors of God do set themselves in array against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Doth the wild ass bray when he hath grass? or loweth the ox over his fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Can that which hath no savour be eaten without salt? or is there any taste in the juice of mallows?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
My soul refuseth to touch them; they are as the sickness of my flesh.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
Oh that I might have my request, and that God would grant me the thing that I long for!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
Even that it would please God to crush me; that He would let loose His hand, and cut me off!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Then should I yet have comfort; yea, I would exult in pain, though He spare not; for I have not denied the words of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What is my strength, that I should wait? and what is mine end, that I should be patient?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength the strength of stones? or is my flesh of brass?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Is it that I have no help in me, and that sound wisdom is driven quite from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
To him that is ready to faint kindness is due from his friend, even to him that forsaketh the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
My brethren have dealt deceitfully as a brook, as the channel of brooks that overflow,
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Which are black by reason of the ice, and wherein the snow hideth itself;
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
What time they wax warm, they vanish, when it is hot, they are consumed out of their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
The paths of their way do wind, they go up into the waste, and are lost.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The caravans of Tema looked, the companies of Sheba waited for them —
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They were ashamed because they had hoped; they came thither, and were confounded.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For now ye are become His; ye see a terror, and are afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Did I say: 'Give unto me'? or: 'Offer a present for me of your substance'?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
or: 'Deliver me from the adversary's hand'? or: 'Redeem me from the hand of the oppressors'?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Teach me, and I will hold my peace; and cause me to understand wherein I have erred.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How forcible are words of uprightness! But what doth your arguing argue?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Do ye hold words to be an argument, but the speeches of one that is desperate to be wind?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Yea, ye would cast lots upon the fatherless, and dig a pit for your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Now therefore be pleased to look upon me; for surely I shall not lie to your face.
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Return, I pray you, let there be no injustice; yea, return again, my cause is righteous.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there injustice on my tongue? Cannot my taste discern crafty devices?

< Ayubu 6 >