< Ayubu 5 >

1 Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
¡Clama ahora! ¿Habrá quién te responda? ¿A cuál de los santos acudirás?
2 Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
Porque la ira mata al necio, y la envidia mata al simple.
3 Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
Vi al necio que echaba raíces, y al instante maldije su vivienda.
4 Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
Sus hijos están lejos de toda seguridad. Son aplastados en la puerta y no habrá quién los defienda.
5 Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
Su cosecha la devoran los hambrientos y aun la sacan de entre los espinos. Los sedientos sorben su hacienda.
6 Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
Porque la aflicción no sale del polvo, ni el sufrimiento brota de la tierra,
7 Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
sino el hombre nace para la aflicción, como las chispas salen hacia arriba.
8 Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
Ciertamente yo buscaría a ʼElohim y encomendaría a Él mi causa,
9 yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
Quien hace cosas grandes e inescrutables, maravillas incontables.
10 Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
Él da la lluvia a la tierra y envía el agua sobre la superficie de los campos.
11 Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
Él exalta a los humildes y levanta a los enlutados a la seguridad.
12 Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
Frustra los pensamientos de los astutos para que nada hagan sus manos y
13 Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
atrapa a los sabios en su astucia. Frustra los designios del perverso.
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
Tropiezan de día con la oscuridad y a mediodía andan a tientas como de noche.
15 Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
Así libra al pobre de la espada, de la boca de los poderosos y de su mano.
16 Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
El necesitado conserva la esperanza. La perversidad cierra su boca.
17 Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
Dichoso el hombre a quien ʼElohim disciplina. No menosprecies la corrección de ʼEL-Shadday,
18 Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
porque Él hace la herida, pero también la venda. Hiere, pero sus manos sanan.
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
Te librará de seis tribulaciones, y aun en la séptima no te tocará el mal.
20 Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
Durante la hambruna te librará de la muerte, y del poder de la espada en la guerra.
21 Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
Estarás escondido del azote de la lengua, y no temerás cuando venga la destrucción.
22 Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
Te reirás de la destrucción y de la hambruna y no temerás a las fieras del campo,
23 Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
pues aun con las piedras del campo harás pacto, y las bestias del campo tendrán paz contigo.
24 Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
Sabrás que hay paz en tu tienda. Nada te faltará cuando revises tu morada.
25 Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
Verás también que tu descendencia es numerosa y tu prole como la hierba de la tierra.
26 Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
Irás a la tumba en la vejez, como la gavilla de trigo que se recoge a su tiempo.
27 Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”
Mira que esto lo investigamos, es así. Óyelo, y conócelo por ti mismo.

< Ayubu 5 >