< Ayubu 5 >

1 Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
«الان استغاثه کن و آیا کسی هست که تو راجواب دهد؟ و به کدامیک از مقدسان توجه خواهی نمود؟۱
2 Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
زیرا غصه، احمق رامی کشد و حسد، ابله را می‌میراند.۲
3 Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
من احمق رادیدم که ریشه می‌گرفت و ناگهان مسکن او رانفرین کردم.۳
4 Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
فرزندان او از امنیت دور هستند ودر دروازه پایمال می‌شوند و رهاننده‌ای نیست.۴
5 Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
که گرسنگان محصول او را می‌خورند، و آن رانیز از میان خارها می‌چینند، و دهان تله برای دولت ایشان باز است.۵
6 Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
زیرا که بلا از غبار درنمی آید، و مشقت از زمین نمی روید.۶
7 Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
بلکه انسان برای مشقت مولود می‌شود، چنانکه شراره‌ها بالامی پرد.۷
8 Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
و لکن من نزد خدا طلب می‌کردم، ودعوی خود را بر خدا می‌سپردم،۸
9 yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
که اعمال عظیم و بی‌قیاس می‌کند و عجایب بی‌شمار؛۹
10 Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
که بر روی زمین باران می‌باراند، و آب بر روی صخره‌ها جاری می‌سازد،۱۰
11 Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
تا مسکینان را به مقام بلند برساند، و ماتمیان به سلامتی سرافراشته شوند.۱۱
12 Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
که فکرهای حیله گران را باطل می‌سازد، به طوری که دستهای ایشان هیچ کار مفیدنمی تواند کرد.۱۲
13 Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
که حکیمان را در حیله ایشان گرفتار می‌سازد، و مشورت مکاران مشوش می‌شود.۱۳
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
در روز به تاریکی برمی خورند و به وقت ظهر، مثل شب کورانه راه می‌روند.۱۴
15 Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
که مسکین را از شمشیر دهان ایشان، و از دست زورآور نجات می‌دهد.۱۵
16 Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
پس امید، برای ذلیل پیدا می‌شود و شرارت دهان خود را می‌بندد.۱۶
17 Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
«هان، خوشابحال شخصی که خدا تنبیهش می‌کند. پس تادیب قادر مطلق را خوار مشمار.۱۷
18 Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
زیرا که او مجروح می‌سازد و التیام می‌دهد، ومی کوبد و دست او شفا می‌دهد.۱۸
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
در شش بلا، تو را نجات خواهد داد و در هفت بلا، هیچ ضرر برتو نخواهد رسید.۱۹
20 Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
در قحط تو را از موت فدیه خواهد داد، و در جنگ از دم شمشیر.۲۰
21 Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
ازتازیانه زبان پنهان خواهی ماند، و چون هلاکت آید، از آن نخواهی ترسید.۲۱
22 Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
بر خرابی وتنگسالی خواهی خندید، و از وحوش زمین بیم نخواهی داشت.۲۲
23 Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
زیرا با سنگهای صحراهمداستان خواهی بود، و وحوش صحرا با توصلح خواهند کرد.۲۳
24 Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
و خواهی دانست که خیمه تو ایمن است، و مسکن خود را تجسس خواهی کرد و چیزی مفقود نخواهی یافت.۲۴
25 Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
وخواهی دانست که ذریتت کثیر است و اولاد تومثل علف زمین.۲۵
26 Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
و در شیخوخیت به قبرخواهی رفت، مثل بافه گندم که در موسمش برداشته می‌شود.۲۶
27 Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”
اینک این را تفتیش نمودیم وچنین است، پس تو این را بشنو و برای خویشتن بدان.»۲۷

< Ayubu 5 >