< Ayubu 5 >

1 Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
Pray, call, is there any to answer thee? And unto which of the holy ones dost thou turn?
2 Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
For provocation slayeth the perverse, And envy putteth to death the simple,
3 Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
I — I have seen the perverse taking root, And I mark his habitation straightway,
4 Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
Far are his sons from safety, And they are bruised in the gate, And there is no deliverer.
5 Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
Whose harvest the hungry doth eat, And even from the thorns taketh it, And the designing swallowed their wealth.
6 Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
For sorrow cometh not forth from the dust, Nor from the ground springeth up misery.
7 Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
For man to misery is born, And the sparks go high to fly.
8 Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
Yet I — I inquire for God, And for God I give my word,
9 yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
Doing great things, and there is no searching. Wonderful, till there is no numbering.
10 Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
Who is giving rain on the face of the land, And is sending waters on the out-places.
11 Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
To set the low on a high place, And the mourners have been high [in] safety.
12 Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
Making void thoughts of the subtile, And their hands do not execute wisdom.
13 Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
Capturing the wise in their subtilty, And the counsel of wrestling ones was hastened,
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
By day they meet darkness, And as night — they grope at noon.
15 Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
And He saveth the wasted from their mouth, And from a strong hand the needy,
16 Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
And there is hope to the poor, And perverseness hath shut her mouth.
17 Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
Lo, the happiness of mortal man, God doth reprove him: And the chastisement of the Mighty despise not,
18 Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
For He doth pain, and He bindeth up, He smiteth, and His hands heal.
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
In six distresses He delivereth thee, And in seven evil striketh not on thee.
20 Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
In famine He hath redeemed thee from death, And in battle from the hands of the sword.
21 Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
When the tongue scourgeth thou art hid, And thou art not afraid of destruction, When it cometh.
22 Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
At destruction and at hunger thou mockest, And of the beast of the earth, Thou art not afraid.
23 Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
(For with sons of the field [is] thy covenant, And the beast of the field Hath been at peace with thee.)
24 Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
And thou hast known that thy tent [is] peace, And inspected thy habitation, and errest not,
25 Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
And hast known that numerous [is] Thy seed, And thine offspring as the herb of the earth;
26 Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
Thou comest in full age unto the grave, As the going up of a stalk in its season.
27 Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”
Lo, this — we searched it out — it [is] right, hearken; And thou, know for thyself!

< Ayubu 5 >