< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
“¿Puedes sacar al Leviatán con un anzuelo? o presionar su lengua con una cuerda?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
¿Puedes poner una cuerda en su nariz, o atravesar su mandíbula con un gancho?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Te hará muchas peticiones, ¿o te hablará con palabras suaves?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Hará un pacto con vosotros, para que lo tomes por siervo para siempre?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
¿Jugarás con él como con un pájaro? ¿O lo atarás para tus chicas?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
¿Los comerciantes harán un trueque por él? ¿Lo repartirán entre los comerciantes?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Puede llenar su piel con hierros de púas, o su cabeza con lanzas de pescado?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Pon tu mano sobre él. Recuerda la batalla, y no lo hagas más.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
He aquí que la esperanza de él es vana. ¿No se abatirá uno incluso al verlo?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Nadie es tan feroz que se atreva a agitarlo. ¿Quién es, pues, el que puede presentarse ante mí?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
¿Quién me ha dado primero, para que yo le pague? Todo bajo el cielo es mío.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
“No guardaré silencio sobre sus miembros, ni su poderosa fuerza, ni su buena contextura.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
¿Quién puede despojarse de su prenda exterior? ¿Quién se acercará a sus fauces?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
¿Quién puede abrir las puertas de su rostro? Alrededor de sus dientes está el terror.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Las fuertes escamas son su orgullo, encerrados juntos con un cierre hermético.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Uno está tan cerca de otro, que ningún aire pueda interponerse entre ellos.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Están unidos entre sí. Se pegan entre sí, de modo que no se pueden separar.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Su estornudo hace brillar la luz. Sus ojos son como los párpados de la mañana.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
De su boca salen antorchas ardientes. Saltan chispas de fuego.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
De sus fosas nasales sale un humo, como de una olla hirviendo sobre un fuego de cañas.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Su aliento enciende las brasas. Una llama sale de su boca.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Hay fuerza en su cuello. El terror baila ante él.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Las escamas de su carne están unidas. Son firmes con él. No se pueden mover.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Su corazón es firme como una piedra, sí, firme como la piedra de molino inferior.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Cuando se levanta, los poderosos tienen miedo. Se retiran ante su paliza.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Si uno lo ataca con la espada, no puede prevalecer; ni la lanza, ni el dardo, ni el asta puntiaguda.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Cuenta el hierro como paja, y el bronce como la madera podrida.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
La flecha no puede hacerle huir. Las piedras de la honda son como la paja para él.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Los palos se cuentan como rastrojos. Se ríe de las prisas de la jabalina.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sus partes inferiores son como alfareros afilados, dejando un rastro en el barro como un trineo.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Hace que lo profundo hierva como una olla. Hace que el mar sea como un bote de pomada.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Hace brillar un camino tras él. Se diría que el profundo tiene el pelo blanco.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
En la tierra no hay nada igual, que se hace sin miedo.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Él ve todo lo que es alto. Es el rey de todos los hijos de la soberbia”.

< Ayubu 41 >