< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Хоћеш ли удицом извући крокодила или ужем подвезати му језик?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Хоћеш ли му провући ситу кроз нос? Или му шиљком провртети чељусти?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Хоће ли те много молити, или ће ти ласкати?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Хоће ли учинити веру с тобом да га узмеш да ти буде слуга до века?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Хоћеш ли се играти с њим као с птицом, или ћеш га везати девојкама својим?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Хоће ли се њим частити другови? Разделити га међу трговце?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Хоћеш ли му напунити кожу шиљцима и главу оствама?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Дигни на њ руку своју; нећеш више помињати боја.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Гле, залуду је надати му се; кад га само угледа човек, не пада ли?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Нема слободног који би га пробудио; а ко ће стати преда ме?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Ко ми је пре дао шта, да му вратим? Шта је год под свим небом, моје је.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Нећу ћутати о удима његовим ни о сили ни о лепоти стаса његовог.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Ко ће му узгрнути горњу одећу? К чељустима његовим ко ће приступити?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Врата грла његовог ко ће отворити? Страх је око зуба његових.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Крљушти су му јаки штитови спојени тврдо.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Близу су једна до друге да ни ветар не улази међу њих.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Једна је за другу прионула, држе се и не растављају се.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Кад киха као да муња сева, а очи су му као трепавице у зоре.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Из уста му излазе лучеви, и искре огњене скачу.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Из ноздрва му излази дим као из врелог лонца или котла.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Дах његов распаљује угљевље и пламен му излази из уста.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
У врату му стоји сила, и пред њим иде страх.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Уди меса његовог спојени су, једноставно је на њему, не размиче се.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Срце му је тврдо као камен, тврдо као доњи жрвањ.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Кад се дигне, дрхћу јунаци, и од страха очишћају се од греха својих.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Да га удари мач, не може се одржати, ни копље ни стрела ни оклоп.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Њему је гвожђе као плева, а бронза као труло дрво.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
Неће га потерати стрела, камење из праће њему је као сламка;
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Као слама су му убојне справе, и смеје се баченом копљу.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Под њим су оштри црепови, стере себи оштре ствари у глибу.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Чини, те ври дубина као лонац, и море се мути као у ступи.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
За собом оставља светлу стазу, рекао би да је бездана оседела.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Ништа нема на земљи да би се испоредило с њим, да би створено било да се ничега не боји.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Шта је год високо презире, цар је над свим зверјем.

< Ayubu 41 >