< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
“Você pode retirar o Leviatã com um anzol de peixe, ou pressionar sua língua com um cordão?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Você pode colocar uma corda em seu nariz, ou trespassar o maxilar com um gancho?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Ele fará muitas petições a você, ou ele lhe dirá palavras suaves?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Ele fará um pacto com você, que você deve tomá-lo por um criado para sempre?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Você vai brincar com ele como com um pássaro? Ou você vai amarrá-lo para suas meninas?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Será que os comerciantes trocarão por ele? Será que eles o dividirão entre os comerciantes?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Can você enche a pele dele com ferros farpados, ou sua cabeça com lanças de peixe?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Lay sua mão sobre ele. Lembre-se da batalha, e não faça mais isso.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Eis que a esperança dele é em vão. Não se vai atirar um para baixo mesmo quando o virmos?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None é tão feroz que ele se atreve a agitá-lo. Quem é então aquele que pode estar diante de mim?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Quem primeiro me deu, para que eu lhe retribuísse? Tudo sob os céus é meu.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
“Não guardarei silêncio a respeito de seus membros, nem sua força poderosa, nem sua boa estrutura.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Quem pode despir sua roupa exterior? Quem vai entrar em suas mandíbulas?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who pode abrir as portas de seu rosto? Ao redor de seus dentes está o terror.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Escalas fortes são seu orgulho, calar junto com um selo apertado.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One está tão perto de outro, que nenhum ar pode ficar entre eles.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They estão unidos uns aos outros. Eles ficam juntos, de modo que não podem ser separados.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Seus espirros piscam. Seus olhos são como as pálpebras da manhã.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out de sua boca vão tochas ardentes. Centelhas de fogo saltam para fora.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Out de suas narinas uma fumaça vai, como de uma panela fervente sobre um fogo de canas.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Seu hálito faz arrepiar os brasas. Uma chama sai de sua boca.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Há força em seu pescoço. O terror dança diante dele.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Os flocos de sua carne são unidos. Eles são firmes com ele. Eles não podem ser movidos.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Seu coração é tão firme como uma pedra, sim, firme como a pedra de moinho inferior.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Quando ele se levanta, os poderosos têm medo. Eles se retiram antes de seu espancamento.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Se alguém o ataca com a espada, ela não pode prevalecer; nem a lança, o dardo, nem o eixo pontiagudo.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He conta o ferro como palha, e bronze como madeira podre.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The seta não pode faze-lo fugir. As pedras de fundição são como palha para ele.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Clubs são contados como restolho. Ele ri da pressa do dardo de arremesso.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
His As partes inferiores são como cacos afiados, deixando um rastro na lama como uma debulhadora.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He faz o fundo ferver como uma panela. Ele faz o mar como um pote de ungüento.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
He faz brilhar um caminho atrás dele. Poder-se-ia pensar que o fundo tinha cabelos brancos.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
On terra lá não é igual a ele, que é feito sem medo.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He vê tudo que é alto. Ele é rei sobre todos os filhos do orgulho”.

< Ayubu 41 >