< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Poderás tu pescar ao leviatã com anzol, ou abaixar sua língua com uma corda?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Podes pôr um anzol em seu nariz, ou com um espinho furar sua queixada?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Fará ele súplicas a ti, [ou] falará contigo suavemente?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Fará ele pacto contigo, para que tu o tomes por escravo perpétuo?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Brincarás tu com ele como com um passarinho, ou o atarás para tuas meninas?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Os companheiros farão banquete dele? Repartirão dele entre os mercadores?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Poderás tu encher sua pele de espetos, ou sua cabeça com arpões de pescadores?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Põe tua mão sobre ele; te lembrarás da batalha, e nunca mais voltarás a fazer.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Eis que a esperança de alguém [de vencê-lo] falhará; pois, apenas ao vê-lo será derrubado.
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Ninguém há [tão] ousado que o desperte; quem pois, [ousa] se opor a mim?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Quem me deu primeiro, para que eu [o] recompense? Tudo o que há debaixo dos céus é meu.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Eu não me calarei a respeito de seus membros, nem de [suas] forças, e da graça de sua estatura.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Quem descobrirá sua vestimenta superficial? Quem poderá penetrar sua couraça dupla?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Quem poderia abrir as portas de seu rosto? Ao redor de seus dentes há espanto.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Seus fortes escudos são excelentes; cada um fechado, como um selo apertado.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Um está tão próximo do outro, que vento não pode entrar entre eles.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Estão grudados uns aos outros; estão tão travados entre si, que não se podem separar.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Cada um de seus roncos faz resplandecer a luz, e seus olhos são como os cílios do amanhecer.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
De sua boca saem tochas, faíscas de fogo saltam dela.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
De suas narinas sai fumaça, como de uma panela fervente ou de um caldeirão.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Seu fôlego acende carvões, e de sua boca sai chama.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
A força habita em seu pescoço; diante dele salta-se de medo.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
As dobras de sua carne estão apegadas [entre si]; cada uma está firme nele, e não podem ser movidas.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Seu coração é rígido como uma pedra, rígido como a pedra de baixo de um moinho.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Quando ele se levanta, os fortes tremem; por [seus] abalos se recuam.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Se alguém lhe tocar com a espada, não poderá prevalecer; nem arremessar dardo, ou lança.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Ele considera o ferro como palha, e o aço como madeira podre.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
A flecha não o faz fugir; as pedras de funda são para ele como sobras de cascas.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Considera toda arma como sobras de cascas, e zomba do mover da lança.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Por debaixo de si tem conchas pontiagudas; ele esmaga com suas pontas na lama.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Ele faz ferver as profundezas como a uma panela, e faz do mar como um pote de unguento.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Ele faz brilhar o caminho atrás de si; faz parecer ao abismo com cabelos grisalhos.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Não há sobre a terra algo que se possa comparar a ele. Ele foi feito para não temer.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Ele vê tudo que é alto; ele é rei sobre todos os filhos dos animais soberbos.

< Ayubu 41 >