< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Poderás tirar com anzol o leviathan? ou ligarás a sua lingua com a corda?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Podes pôr um junco no seu nariz? ou com um espinho furarás a sua queixada?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Porventura multiplicará muitas supplicações para comtigo? ou brandamente fallará?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Fará elle concertos comtigo? ou o tomarás tu por escravo para sempre?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Brincarás com elle, como com um passarinho? ou o atarás para tuas meninas?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Os teus companheiros farão d'elle um banquete? ou o repartirão entre os negociantes?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Encherás a sua pelle de ganchos? ou a sua cabeça com arpéos de pescadores?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Põe a tua mão sobre elle, lembra-te da peleja, e nunca mais tal intentarás.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Eis que a sua esperança falhará: porventura tambem á sua vista será derribado?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Ninguem ha tão atrevido, que a despertal-o se atreva: quem pois é aquelle que ousa pôr-se em pé diante de mim
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Quem me preveniu, para que eu haja de retribuir-lhe? pois o que está debaixo de todos os céus é meu.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Não calarei os meus membros, nem a relação das suas forças, nem a graça da sua formação.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Quem descobriria a superficie do seu vestido? quem entrará entre as suas queixadas dobradas?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Quem abriria as portas do seu rosto? pois em roda dos seus dentes está o terror.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
As suas fortes escamas são excellentissimas, cada uma fechada como com sello apertado.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Uma á outra se chega tão perto, que nem um assopro passa por entre ellas.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Umas ás outras se apegam: tanto se travam entre si, que não se podem separar.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Cada um dos seus espirros faz resplandecer a luz, e os seus olhos são como as pestanas da alva.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Da sua bocca saem tochas: faiscas de fogo arrebentam d'ella.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Dos seus narizes procede fumo, como d'uma panella fervente, ou d'uma grande caldeira.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
O seu halito faria incender os carvões: e da sua bocca sae chamma.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
No seu pescoço pousa a força: perante elle até a tristeza salta de prazer.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Os musculos da sua carne estão pegados entre si: cada um está firme n'elle, e nenhum se move.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
O seu coração é firme como uma pedra e firme como parte da mó de baixo.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Levantando-se elle, tremem os valentes: em razão dos seus abalos se purificam.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Se alguem lhe tocar com a espada, essa não poderá penetrar, nem lança, dardo ou couraça.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Elle reputa o ferro por palha, e o cobre por pau podre.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
A setta o não fará fugir: as pedras das fundas se lhe tornam em rastolho.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
As pedras atiradas estima como arestas, e ri-se do brandir da lança.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Debaixo de si tem conchas ponteagudas: estende-se sobre coisas ponteagudas como na lama.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
As profundezas faz ferver, como uma panella: torna o mar como quando os unguentos fervem.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Apoz elle allumia o caminho: parece o abysmo tornado em brancura de cãs.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Na terra não ha coisa que se lhe possa comparar, pois foi feito para estar sem pavor.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Todo o alto vê: é rei sobre todos os filhos d'animaes altivos.

< Ayubu 41 >