< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Czy lewiatana wyciągniesz wędką? Czy za jego język [wyciągniesz go] sznurem opuszczonym?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Czy przewleczesz hak przez jego nozdrza? Czy kolcem przebijesz mu szczęki?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Czy będzie cię błagać? Czy będzie z tobą rozmawiał łagodnie?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Czy zawrze z tobą przymierze? Czy przyjmiesz go za sługę na zawsze?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Czy będziesz z nim igrał jak z ptaszkiem? Czy uwiążesz go dla swoich córek?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Czy [twoi] towarzysze wyprawią sobie z niego ucztę? Czy podzielą go między siebie kupcy?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Czy poprzebijasz jego skórę grotami albo jego głowę harpunami?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Połóż tylko rękę na niego i wspomnij o walce, więcej tego nie zrobisz.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Oto nadzieja pojmania go jest złudna. Czy na sam jego widok nie zostanie człowiek powalony?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Nikt nie odważy się go obudzić. Kto zdoła więc stanąć przede mną?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Kto mi coś dał, abym mu odpłacił? [Cokolwiek znajduje się] pod całym niebem należy do mnie.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Nie będę milczał o jego członkach ani o jego potędze, ani o jego wspaniałej budowie.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Kto odkryje wierzch jego szaty? Kto przystąpi [do niego] z podwójnym wędzidłem?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Kto otworzy wrota jego paszczy? Groza roztacza się wokół jego zębów.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
[Jego] łuski to jego pycha, ściśle spięte razem [jakby] pieczęcią.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Jedna do drugiej tak przylega, że powietrze nie wejdzie między nie.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Jedna z drugą jest spojona, są tak złączone, że nie można ich rozdzielić.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Przez jego kichanie błyszczy światło, a jego oczy [są] jak powieki zorzy.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Z jego paszczy wychodzą pochodnie, tryskają iskry ognia.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Z jego nozdrzy wychodzi dym jak z wrzącego garnca lub kotła.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Jego oddech rozpala węgle, z jego paszczy wychodzi płomień.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
W jego szyi spoczywa moc i przed nim ucieka smutek.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Warstwy jego ciała są spojone, tak twarde, że się nie poruszają.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Jego serce jest twarde jak kamień, tak twarde jak część dolnego kamienia młyńskiego.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Gdy się podnosi, drżą mocarze, a od strachu oczyszczają się.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Miecz, który go dosięga, nie ostaje się, podobnie drzewce, strzała i pancerz.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Żelazo uważa za słomę, a miedź za zbutwiałe drewno.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
Strzała nie spłoszy go, a kamienie z procy są dla niego jak źdźbło.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Oszczep uważa za słomę, a drwi sobie z szarpania włócznią.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Pod nim [są] ostre skorupy; w błocie ścieli [sobie wszelkimi] ostrymi rzeczami.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Sprawia, że głębiny wrą jak kocioł, a morze mąci jak w moździerzu.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Zostawia za sobą błyszczącą ścieżkę, tak że się wydaje, że głębiny mają siwiznę.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Nie ma na ziemi jemu podobnego, który został tak stworzony, że niczego się nie boi.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Lekceważy wszelką wysoką rzecz. On jest królem nad wszystkimi synami pychy.

< Ayubu 41 >