< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
An extrahere poteris Leviathan hamo, et fune ligabis linguam ejus?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Numquid pones circulum in naribus ejus, aut armilla perforabis maxillam ejus?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Numquid multiplicabit ad te preces, aut loquetur tibi mollia?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Numquid feriet tecum pactum, et accipies eum servum sempiternum?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Numquid illudes ei quasi avi, aut ligabis eum ancillis tuis?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Concident eum amici? divident illum negotiatores?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Numquid implebis sagenas pelle ejus, et gurgustium piscium capite illius?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Pone super eum manum tuam: memento belli, nec ultra addas loqui.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Ecce spes ejus frustrabitur eum, et videntibus cunctis præcipitabitur.
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Non quasi crudelis suscitabo eum: quis enim resistere potest vultui meo?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Quis ante dedit mihi, ut reddam ei? omnia quæ sub cælo sunt, mea sunt.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Non parcam ei, et verbis potentibus, et ad deprecandum compositis.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Quis revelabit faciem indumenti ejus? et in medium oris ejus quis intrabit?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Portas vultus ejus quis aperiet? per gyrum dentium ejus formido.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Corpus illius quasi scuta fusilia, compactum squamis se prementibus.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Una uni conjungitur, et ne spiraculum quidem incedit per eas.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Una alteri adhærebit, et tenentes se nequaquam separabuntur.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Sternutatio ejus splendor ignis, et oculi ejus ut palpebræ diluculi.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
De ore ejus lampades procedunt, sicut tædæ ignis accensæ.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
De naribus ejus procedit fumus, sicut ollæ succensæ atque ferventis.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Halitus ejus prunas ardere facit, et flamma de ore ejus egreditur.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
In collo ejus morabitur fortitudo, et faciem ejus præcedit egestas.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Membra carnium ejus cohærentia sibi: mittet contra eum fulmina, et ad locum alium non ferentur.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Cor ejus indurabitur tamquam lapis, et stringetur quasi malleatoris incus.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Cum sublatus fuerit, timebunt angeli, et territi purgabuntur.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Cum apprehenderit eum gladius, subsistere non poterit, neque hasta, neque thorax:
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
reputabit enim quasi paleas ferrum, et quasi lignum putridum æs.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
Non fugabit eum vir sagittarius: in stipulam versi sunt ei lapides fundæ.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Quasi stipulam æstimabit malleum, et deridebit vibrantem hastam.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sub ipso erunt radii solis, et sternet sibi aurum quasi lutum.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Fervescere faciet quasi ollam profundum mare, et ponet quasi cum unguenta bulliunt.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Post eum lucebit semita: æstimabit abyssum quasi senescentem.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Non est super terram potestas quæ comparetur ei, qui factus est ut nullum timeret.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Omne sublime videt: ipse est rex super universos filios superbiæ.

< Ayubu 41 >