< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Prendras-tu le crocodile à l’hameçon? Saisiras-tu sa langue avec une corde?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Mettras-tu un jonc dans ses narines? Lui perceras-tu la mâchoire avec un crochet?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Te pressera-t-il de supplication? Te parlera-t-il d’une voix douce?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Fera-t-il une alliance avec toi, Pour devenir à toujours ton esclave?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Joueras-tu avec lui comme avec un oiseau? L’attacheras-tu pour amuser tes jeunes filles?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Les pêcheurs en trafiquent-ils? Le partagent-ils entre les marchands?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Couvriras-tu sa peau de dards, Et sa tête de harpons?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Dresse ta main contre lui, Et tu ne t’aviseras plus de l’attaquer.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Voici, on est trompé dans son attente; A son seul aspect n’est-on pas terrassé?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Nul n’est assez hardi pour l’exciter; Qui donc me résisterait en face?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
De qui suis-je le débiteur? Je le paierai. Sous le ciel tout m’appartient.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Je veux encore parler de ses membres, Et de sa force, et de la beauté de sa structure.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Qui soulèvera son vêtement? Qui pénétrera entre ses mâchoires?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Qui ouvrira les portes de sa gueule? Autour de ses dents habite la terreur.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Ses magnifiques et puissants boucliers Sont unis ensemble comme par un sceau;
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Ils se serrent l’un contre l’autre, Et l’air ne passerait pas entre eux;
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Ce sont des frères qui s’embrassent, Se saisissent, demeurent inséparables.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Ses éternuements font briller la lumière; Ses yeux sont comme les paupières de l’aurore.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Des flammes jaillissent de sa bouche, Des étincelles de feu s’en échappent.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Une fumée sort de ses narines, Comme d’un vase qui bout, d’une chaudière ardente.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Son souffle allume les charbons, Sa gueule lance la flamme.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
La force a son cou pour demeure, Et l’effroi bondit au-devant de lui.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Ses parties charnues tiennent ensemble, Fondues sur lui, inébranlables.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Son cœur est dur comme la pierre, Dur comme la meule inférieure.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Quand il se lève, les plus vaillants ont peur, Et l’épouvante les fait fuir.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
C’est en vain qu’on l’attaque avec l’épée; La lance, le javelot, la cuirasse, ne servent à rien.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Il regarde le fer comme de la paille, L’airain comme du bois pourri.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
La flèche ne le met pas en fuite, Les pierres de la fronde sont pour lui du chaume.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Il ne voit dans la massue qu’un brin de paille, Il rit au sifflement des dards.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sous son ventre sont des pointes aiguës: On dirait une herse qu’il étend sur le limon.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Il fait bouillir le fond de la mer comme une chaudière, Il l’agite comme un vase rempli de parfums.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Il laisse après lui un sentier lumineux; L’abîme prend la chevelure d’un vieillard.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Sur la terre nul n’est son maître; Il a été créé pour ne rien craindre.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Il regarde avec dédain tout ce qui est élevé, Il est le roi des plus fiers animaux.

< Ayubu 41 >