< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
“Can you draw out Leviathan with a fish hook, or press down his tongue with a cord?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Can you put a rope into his nose, or pierce his jaw through with a hook?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he make many petitions to you, or will he speak soft words to you?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Will he make a covenant with you, that you should take him for a servant forever?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Will you play with him as with a bird? Or will you bind him for your girls?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Will traders barter for him? Will they part him amongst the merchants?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Can you fill his skin with barbed irons, or his head with fish spears?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Lay your hand on him. Remember the battle, and do so no more.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Behold, the hope of him is in vain. Won’t one be cast down even at the sight of him?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None is so fierce that he dare stir him up. Who then is he who can stand before me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who has first given to me, that I should repay him? Everything under the heavens is mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
“I will not keep silence concerning his limbs, nor his mighty strength, nor his goodly frame.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who can strip off his outer garment? Who will come within his jaws?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who can open the doors of his face? Around his teeth is terror.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Strong scales are his pride, shut up together with a close seal.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One is so near to another, that no air can come between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They are joined to one another. They stick together, so that they can’t be pulled apart.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezing flashes out light. His eyes are like the eyelids of the morning.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth go burning torches. Sparks of fire leap out.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Out of his nostrils a smoke goes, as of a boiling pot over a fire of reeds.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath kindles coals. A flame goes out of his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
There is strength in his neck. Terror dances before him.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flakes of his flesh are joined together. They are firm on him. They can’t be moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart is as firm as a stone, yes, firm as the lower millstone.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
When he raises himself up, the mighty are afraid. They retreat before his thrashing.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
If one attacks him with the sword, it can’t prevail; nor the spear, the dart, nor the pointed shaft.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He counts iron as straw, and bronze as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The arrow can’t make him flee. Sling stones are like chaff to him.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Clubs are counted as stubble. He laughs at the rushing of the javelin.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
His undersides are like sharp potsherds, leaving a trail in the mud like a threshing sledge.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He makes the deep to boil like a pot. He makes the sea like a pot of ointment.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
He makes a path shine after him. One would think the deep had white hair.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
On earth there is not his equal, that is made without fear.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He sees everything that is high. He is king over all the sons of pride.”

< Ayubu 41 >