< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Can you draw out leviathan (sea serpent) with an hook? or his tongue with a cord which you let down?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Can you put an hook into his nose? or bore his jaw through with a thorn?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he make many supplications unto you? will he speak soft words unto you?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Will he make a covenant with you? will you take him for a servant for ever?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Will you play with him as with a bird? or will you bind him for your maidens?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Shall the companions make a banquet of him? shall they part him among the merchants?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Can you fill his skin with barbed irons? or his head with fish spears?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Lay your hand upon him, remember the battle, do no more.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Behold, the hope of him is in vain: shall not one be cast down even at the sight of him?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None is so fierce that dare stir him up: who then is able to stand before me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who has prevented me, that I should repay him? whatsoever is under the whole heaven is mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I will not conceal his parts, nor his power, nor his comely proportion.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who can discover the face of his garment? or who can come to him with his double bridle?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who can open the doors of his face? his teeth are terrible round about.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
His scales are his pride, shut up together as with a close seal.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One is so near to another, that no air can come between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They are joined one to another, they stick together, that they cannot be sundered.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
By his exhaling a light does shine, and his eyes are like the eyelids of the morning.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth go burning lamps, and sparks of fire leap out.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Out of his nostrils goes smoke, as out of a seething pot or caldron.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath kindles coals, and a flame goes out of his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
In his neck remains strength, and sorrow is turned into joy before him.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flakes of his flesh are joined together: they are firm in themselves; they cannot be moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart is as firm as a stone; yea, as hard as a piece of the nether millstone.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
When he raises up himself, the mighty are afraid: by reason of breakings they purify themselves.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
The sword of him that lays at him cannot hold: the spear, the dart, nor the armour of jacket.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He esteems iron as straw, and brass as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The arrow cannot make him flee: sling stones are turned with him into stubble.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Darts are counted as stubble: he laughs at the shaking of a spear.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sharp stones are under him: he spreads sharp pointed things upon the mire.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He makes the deep to boil like a pot: he makes the sea like a pot of ointment.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
He makes a path to shine after him; one would think the deep to be hoary.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Upon earth there is not his like, who is made without fear.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He beholds all high things: he is a king over all the children of pride.

< Ayubu 41 >