< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Is it possible for Leviathan to be pulled out with a fish-hook, or for a hook to be put through the bone of his mouth?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Will you put a cord into his nose, or take him away with a cord round his tongue?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he make prayers to you, or say soft words to you?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Will he make an agreement with you, so that you may take him as a servant for ever?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Will you make sport with him, as with a bird? or put him in chains for your young women?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Will the fishermen make profit out of him? will they have him cut up for the traders?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Will you put sharp-pointed irons into his skin, or fish-spears into his head?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Only put your hand on him, and see what a fight you will have; you will not do it again!
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Truly, the hope of his attacker is false; he is overcome even on seeing him!
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
He is so cruel that no one is ready to go against him. Who then is able to keep his place before me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who ever went against me, and got the better of me? There is no one under heaven!
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I will not keep quiet about the parts of his body, or about his power, and the strength of his frame.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who has ever taken off his outer skin? who may come inside his inner coat of iron?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who has made open the doors of his face? Fear is round about his teeth.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
His back is made of lines of plates, joined tight together, one against the other, like a stamp.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One is so near to the other that no air may come between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They take a grip of one another; they are joined together, so that they may not be parted.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezings give out flames, and his eyes are like the eyes of the dawn.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth go burning lights, and flames of fire are jumping up.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Smoke comes out of his nose, like a pot boiling on the fire.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath puts fire to coals, and a flame goes out of his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Strength is in his neck, and fear goes dancing before him.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The plates of his flesh are joined together, fixed, and not to be moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart is as strong as a stone, hard as the lower crushing-stone.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
When he gets ready for the fight, the strong are overcome with fear.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
The sword may come near him but is not able to go through him; the spear, or the arrow, or the sharp-pointed iron.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Iron is to him as dry grass, and brass as soft wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The arrow is not able to put him to flight: stones are no more to him than dry stems.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
A thick stick is no better than a leaf of grass, and he makes sport of the onrush of the spear.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Under him are sharp edges of broken pots: as if he was pulling a grain-crushing instrument over the wet earth.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
The deep is boiling like a pot of spices, and the sea like a perfume-vessel.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
After him his way is shining, so that the deep seems white.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
On earth there is not another like him, who is made without fear.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Everything which is high goes in fear of him; he is king over all the sons of pride.

< Ayubu 41 >