< Ayubu 4 >

1 Kisha Elifazi Mtemani akajibu na kusema,
その時、テマンびとエリパズが答えて言った、
2 Kama mtu yeyote akijaribu kuzungumza na wewe, je utakosa ustahimilivu? Lakini ni nani anaweza kujizuia asizungumze?
「もし人があなたにむかって意見を述べるならば、あなたは腹を立てるでしょうか。しかしだれが黙っておれましょう。
3 Tazama, wewe umewafunza wengi; wewe imeipa nguvu mikono iliyokuwa dhaifu.
見よ、あなたは多くの人を教えさとし、衰えた手を強くした。
4 Maneno yako yamemsaidia yeye mwanamme aliyekuwa anaanguka; wewe umeyaimarisha magoti dhaifu.
あなたの言葉はつまずく者をたすけ起し、かよわいひざを強くした。
5 Lakini sasa matatizo yamekuja kwako, na wewe umechoka; yanakugusa wewe, na wewe umetatizika.
ところが今、この事があなたに臨むと、あなたは耐え得ない。この事があなたに触れると、あなたはおじ惑う。
6 Je si hofu yako imani yako, na ukamilifu wa njia zako tumaini lako?
あなたが神を恐れていることは、あなたのよりどころではないか。あなたの道の全きことは、あなたの望みではないか。
7 Tafakari juu ya hili, tafadhari: ni nani aliyeangamia akiwa hana kosa? Au ni lini watu wakamilifu walikatiliwa mbali?
考えてみよ、だれが罪のないのに、滅ぼされた者があるか。どこに正しい者で、断ち滅ぼされた者があるか。
8 Kutokana na vile nilivyoona, wale walimao uovu na kupanda taabu huvuna hayo.
わたしの見た所によれば、不義を耕し、害悪をまく者は、それを刈り取っている。
9 Kwa pumzi ya Mungu huangamia; kwa mlipuko wa hasira zake huteketea.
彼らは神のいぶきによって滅び、その怒りの息によって消えうせる。
10 Kuunguruma kwa simba, sauti ya simba mkali, meno ya simba wadogo - yamevunjika.
ししのほえる声、たけきししの声はともにやみ、若きししのきばは折られ、
11 Simba mzee huangamia kwa kukosa wahanga; watoto wa simba jike wametawanyiko kila mahali.
雄じしは獲物を得ずに滅び、雌じしの子は散らされる。
12 Sasa nililetewa kwangu jambo fulani kisiri, na sikio langu likapokea uvumi kuhusu hilo.
さて、わたしに、言葉がひそかに臨んだ、わたしの耳はそのささやきを聞いた。
13 Kisha yakaja mawazo kupitia ndoto wakati wa usiku, wakati uwaangukiwapo usingizi mzito watu.
すなわち人の熟睡するころ、夜の幻によって思い乱れている時、
14 Ilikuwa usiku wakati nilipopatwa hofu na kutetemeka, na mifupa yangu yote ikatikisika.
恐れがわたしに臨んだので、おののき、わたしの骨はことごとく震えた。
15 Kisha nafsi ikapita mbele ya uso wangu, na nywele zangu za mwili zilisimama.
時に、霊があって、わたしの顔の前を過ぎたので、わたしの身の毛はよだった。
16 Nafsi ilisimama kimya, lakini sikuweza kupambanua sura yake. Umbo lilikuwa mbele ya macho yangu; kulikuwa kimya, nami nikasikia sauti ikisema,
そのものは立ちどまったが、わたしはその姿を見わけることができなかった。一つのかたちが、わたしの目の前にあった。わたしは静かな声を聞いた、
17 “Je binadamu anaweza kuwa mwenye haki zaidi kuliko Mungu? Je mtu anaweza kuwa msafi zaidi kuliko muumba wake?
『人は神の前に正しくありえようか。人はその造り主の前に清くありえようか。
18 Tazama, kama Mungu hawaamini watumishi wake; kama hulaumu upumbavu wa malaika zake,
見よ、彼はそのしもべをさえ頼みとせず、その天使をも誤れる者とみなされる。
19 je si zaidi sana ukweli huu kwa wale waishio katika nyumba za udongo, ambao misingi yao ipo katika vumbi, wale waliopondwa mbele ya nondo?
まして、泥の家に住む者、ちりをその基とする者、しみのようにつぶされる者。
20 Kati ya asubuhi na jioni wameangamizwa; wameangamia milele wala bila yeyote kuwatambua.
彼らは朝から夕までの間に打ち砕かれ、顧みる者もなく、永遠に滅びる。
21 Je kamba za hema yao hazikung'olewa kati yao? Wanakufa; wanakufa bila hekima.
もしその天幕の綱が彼らのうちに取り去られるなら、ついに悟ることもなく、死にうせるではないか』。

< Ayubu 4 >