< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao? 2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao? 3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi. 4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena. 5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi, 6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi? 7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji. 8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula. 9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako? 10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako? 11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye? 12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria? 13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo? 14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi; 15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga. 16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure, 17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote. 18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake. 19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya? 20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha. 21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha. 22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga. 23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo. 24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja. 25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele. 26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini? 27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu? 28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni. 29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali. 30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Ayubu 39 >