< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
Hast thou known the time of The bearing of the wild goats of the rock? The bringing forth of hinds thou dost mark!
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Thou dost number the months they fulfil? And thou hast known the time of their bringing forth!
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
They bow down, Their young ones they bring forth safely, Their pangs they cast forth.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Safe are their young ones, They grow up in the field, they have gone out, And have not returned to them.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Who hath sent forth the wild ass free? Yea, the bands of the wild ass who opened?
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
Whose house I have made the wilderness, And his dwellings the barren land,
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
He doth laugh at the multitude of a city, The cries of an exactor he heareth not.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
The range of mountains [is] his pasture, And after every green thing he seeketh.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
Is a Reem willing to serve thee? Doth he lodge by thy crib?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
Dost thou bind a Reem in a furrow [with] his thick band? Doth he harrow valleys after thee?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
Dost thou trust in him because great [is] his power? And dost thou leave unto him thy labour?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
Dost thou trust in him That he doth bring back thy seed? And [to] thy threshing-floor doth gather [it]?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
The wing of the rattling ones exulteth, Whether the pinion of the ostrich or hawk.
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
For she leaveth on the earth her eggs, And on the dust she doth warm them,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
And she forgetteth that a foot may press it, And a beast of the field tread it down.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
Her young ones it hath hardened without her, In vain [is] her labour without fear.
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
For God hath caused her to forget wisdom, And He hath not given a portion To her in understanding:
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
At the time on high she lifteth herself up, She laugheth at the horse and at his rider.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Dost thou give to the horse might? Dost thou clothe his neck [with] a mane?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
Dost thou cause him to rush as a locust? The majesty of his snorting [is] terrible.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
They dig in a valley, and he rejoiceth in power, He goeth forth to meet the armour.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
He laugheth at fear, and is not affrighted, And he turneth not back from the face of the sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
Against him rattle doth quiver, The flame of a spear, and a halbert.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
With trembling and rage he swalloweth the ground, And remaineth not stedfast Because of the sound of a trumpet.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
Among the trumpets he saith, Aha, And from afar he doth smell battle, Roaring of princes and shouting.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
By thine understanding flieth a hawk? Spreadeth he his wings to the south?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
At thy command goeth an eagle up high? Or lifteth he up his nest?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
A rock he doth inhabit, Yea, he lodgeth on the tooth of a rock, and fortress.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
From thence he hath sought food, To a far off place his eyes look attentively,
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
And his brood gulp up blood, And where the pierced [are] — there [is] he!

< Ayubu 39 >