< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
[Say] if you know the time of the bringing forth of the wild goats of the rock, and [if] you have marked the calving of the hinds:
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
and [if] you has have numbered the full months of their being with young, and [if] you have relieved their pangs:
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
and have reared their young without fear; and will you loosen their pangs?
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Their young will break forth; they will be multiplied with offspring: [their young] will go forth, and will not return to them.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
And who is he that sent forth the wild ass free? and who loosed his bands?
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
whereas I made his habitation the wilderness, and the salt land his coverts.
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
He laughs to scorn the multitude of the city, and hears not the chiding of the tax-gatherer.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
He will survey the mountains [as] his pasture, and he seeks after every green thing.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
And will the unicorn be willing to serve you, or to lie down at your manger?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
And will you bind his yoke with thongs, or will he plow furrows for you in the plain?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
And do you trust him, because his strength is great? and will you commit your works to him?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
And will you believe that he will return to you your seed, and bring [it] in [to] your threshing floor?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
The peacock has a beautiful wing: if the stork and the ostrich conceive, [it is worthy of notice],
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
for [the ostrich] will leave her eggs in the ground, and warm them on the dust,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
and has forgotten that the foot will scatter them, and the wild beasts of the field trample them.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
She has hardened [herself] against her young ones, as though [she bereaved] not herself: she labors in vain without fear.
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
For God has withholden wisdom from her, and not given her a portion in understanding.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
In her season she will lift herself on high; she will scorn the horse and his rider.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Hast you invested the horse with strength, and clothed his neck with terror?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
And have you clad him in perfect armor, and made his breast glorious with courage?
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
He paws exulting in the plain, and goes forth in strength into the plain.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
He laughs to scorn a king as he meets him, and will by no means turn back from the sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
The bow and sword resound against him; and [his] rage will swallow up the ground:
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
and he will not believe until the trumpet sounds.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
And when the trumpet sounds, he says, Aha! and afar off he smells the war with prancing and neighing.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
And does the hawk remain steady by your wisdom, having spread out her wings unmoved, looking toward the region of the south?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
And does the eagle rise at your command, and the vulture remain sitting over his nest,
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
on a crag of a rock, and in a secret [place]?
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
Thence he seeks food, his eyes observe from far.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
And his young ones roll themselves in blood, and wherever the carcasses may be, immediately they are found.

< Ayubu 39 >