< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Yavé respondió a Job desde un remolino de viento:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
¿Quién es el que oscurece el consejo con palabras sin entendimiento?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Ciñe ahora tu cintura como varón. Yo te preguntaré, y tú me responderás:
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
¿Dónde estabas tú cuando Yo fundaba la tierra? Dí, si tienes entendimiento.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
¿Quién determinó sus medidas? Con seguridad lo sabes. ¿Quién extendió cordel sobre ella?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
¿Sobre qué están fundados sus cimientos? ¿Quién colocó su piedra angular,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
cuando las estrellas del alba alababan juntas, y todos los hijos de ʼElohim gritaban de júbilo?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
¿Quién encerró al mar con compuertas cuando se salía de su seno?
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
Cuando le coloqué nubes como ropa, y densa oscuridad como envoltura,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
cuando establecí sobre él mi límite, coloqué barra en sus puertas
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
y le dije: Hasta aquí llegarás y no pasarás. Aquí se detendrá el orgullo de tus olas.
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
¿Alguna vez en tu vida diste orden a la mañana? ¿Mostraste a la aurora su lugar?
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
A fin de que tome los confines de la tierra y sacuda de ella a los perversos,
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
sea cambiada como arcilla modelada por el sello, y adelgazada hasta ser como una ropa multicolor,
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
para que se retenga la luz de los perversos y sea quebrado el brazo enaltecido.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
¿Penetraste tú hasta las fuentes del mar o caminaste en las profundidades del abismo?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
¿Te fueron reveladas las puertas de la muerte? ¿Viste las puertas de la profunda oscuridad?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
¿Consideraste tú la anchura de la tierra? Declara si sabes todo esto.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
¿Dónde está el camino hacia la morada de la luz? ¿Dónde vive la oscuridad,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
para que las conduzcas a su territorio y les muestres las sendas a su vivienda?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Tú lo sabes, porque entonces ya habías nacido y el número de tus días es grande.
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
¿Estuviste en los tesoros de la nieve o viste los tesoros del granizo
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
que tengo reservados para el tiempo de angustia, para el día de la guerra y de la batalla?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
¿Por cuál camino se reparte la luz y se esparce el viento del este sobre la tierra?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
¿Quién le abrió cauce al aluvión y camino a los relámpagos y truenos,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
para saciar la tierra deshabitada y desolada, para que brote la hierba,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
para saciar las tierras desoladas, y hacer que broten las semillas de la hierba?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
¿La lluvia tiene padre? ¿Quién engendró las gotas de rocío?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
¿De cuál vientre salió el hielo? ¿Quién engendró la escarcha del cielo
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
para que las aguas se cubran con una losa, que aprisiona la superficie del abismo?
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
¿Podrás anudar las cadenas de las Pléyades o desatar las ligaduras de Orión?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
¿Sacarás las constelaciones del cielo a su tiempo o guiarás la Osa Mayor con sus hijos?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
¿Conoces tú los Estatutos del cielo? ¿Puedes establecer su dominio en la tierra?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
¿Alzarás tu voz hacia las nubes para que te cubra el chaparrón?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
¿Enviarás tú los relámpagos para que vengan y te digan: Aquí estamos?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
¿Quién colocó entendimiento en el ser íntimo? ¿Quién dio entendimiento a la mente?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
¿Quién cuenta las nubes con sabiduría y voltea los cántaros del cielo,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
cuando el polvo se convierte en una masa y los terrones se pegan entre sí?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
¿Cazarás tú presa para la leona? ¿Saciarás el hambre de sus leoncillos
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
cuando están echados en sus cuevas o se agazapan en sus guaridas para acechar?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
¿Quién provee al cuervo su comida, cuando sus pichones claman a ʼElohim mientras vagan sin alimento?

< Ayubu 38 >