< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Und der HERR antwortete Hiob aus einem Wetter und sprach:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Wer ist der, der so fehlet in der Weisheit und redet so mit Unverstand?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gürte deine Lenden wie ein Mann; ich will dich fragen, lehre mich!
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Wo warest du, da ich die Erde gründete? Sage mir's, bist du so klug?
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Weißt du, wer ihr das Maß gesetzt hat, oder wer über sie eine Richtschnur gezogen hat?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Oder worauf stehen ihre Füße versenket? Oder wer hat ihr einen Eckstein gelegt,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
da mich die Morgensterne miteinander lobeten, und jauchzeten alle Kinder Gottes?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Wer hat das Meer mit seinen Türen verschlossen, da es herausbrach wie aus Mutterleibe,
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
da ich's mit Wolken kleidete und in Dunkel einwickelte, wie in Windeln,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
da ich ihm den Lauf brach mit meinem Damm und setzte ihm Riegel und Tür
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
und sprach: Bis hieher sollst du kommen und nicht weiter; hie sollen sich legen deine stolzen Wellen!?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Hast du bei deiner Zeit dem Morgen geboten und der Morgenröte ihren Ort gezeiget,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
daß die Ecken der Erde gefasset und die Gottlosen herausgeschüttelt würden?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Das Siegel wird sich wandeln wie Leimen, und sie stehen wie ein Kleid.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
Und den Gottlosen wird ihr Licht genommen werden; und der Arm der Hoffärtigen wird zerbrochen werden.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Bist du in den Grund des Meers kommen und hast in den Fußtapfen der Tiefen gewandelt?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Haben sich dir des Todes Tore je aufgetan? Oder hast du gesehen die Tore der Finsternis?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Hast du vernommen, wie breit die Erde sei? Sage an, weißt du solches alles?
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Welches ist der Weg, da das Licht wohnet, und welches sei der Finsternis Stätte,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
daß du mögest abnehmen seine Grenze und merken den Pfad zu seinem Hause?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Wußtest du, daß du zu der Zeit solltest geboren werden und wieviel deiner Tage sein würden?
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Bist du gewesen, da der Schnee herkommt, oder hast du gesehen, wo der Hagel herkommt,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
die ich habe verhalten bis auf die Zeit der Trübsal und auf den Tag des Streits und Kriegs?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Durch welchen Weg teilet sich das Licht, und auffähret der Ostwind auf Erden?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Wer hat dem Platzregen seinen Lauf ausgeteilet und den Weg dem Blitze und Donner,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
daß es regnet aufs Land, da niemand ist, in der Wüste, da kein Mensch ist,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
daß er füllet die Einöden und Wildnis und macht, daß Gras wächset?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Wer ist des Regens Vater? Wer hat die Tropfen des Taues gezeuget?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Aus wes Leibe ist das Eis gegangen? Und wer hat den Reif unter dem Himmel gezeuget,
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
daß das Wasser verborgen wird wie unter Steinen und die Tiefe oben gestehet?
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Kannst du die Bande der sieben Sterne zusammenbinden, oder das Band des Orion auflösen?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Kannst du den Morgenstern hervorbringen zu seiner Zeit, oder den Wagen am Himmel über seine Kinder führen?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Weißt du, wie der Himmel zu regieren ist? Oder kannst du ihn meistern auf Erden?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Kannst du deinen Donner in der Wolke hoch herführen? Oder wird dich die Menge des Wassers verdecken?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Kannst du die Blitze auslassen, daß sie hinfahren und sprechen: Hie sind wir?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Wer gibt die Weisheit ins Verborgene? Wer gibt verständige Gedanken?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Wer ist so weise, der die Wolken erzählen könnte? Wer kann die Wasserschläuche am Himmel verstopfen,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
wenn der Staub begossen wird, daß er zuhaufe läuft und die Klöße aneinander kleben?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Kannst du der Löwin ihren Raub zu jagen geben und die jungen Löwen sättigen,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
daß sie sich legen in ihre Stätte und ruhen in der Höhle, da sie lauern?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Wer bereitet dem Raben die Speise, wenn seine Jungen zu Gott rufen und fliegen irre, wenn sie nicht zu essen haben?

< Ayubu 38 >