< Ayubu 37 >

1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
At this also my heart trembleth, and is moved out of its place.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Hearken ye unto the noise of his voice, and the sound that goeth out of his mouth.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
He sendeth it forth under the whole heaven, and his lightning unto the ends of the earth.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
After it a voice roareth; he thundereth with the voice of his majesty: and he stayeth them not when his voice is heard.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
God thundereth marvelously with his voice; great things doeth he, which we cannot comprehend.
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
For he saith to the snow, Fall thou on the earth; likewise to the shower of rain, and to the showers of his mighty rain.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
He sealeth up the hand of every man; that all men whom he hath made may know [it].
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
Then the beasts go into coverts, and remain in their dens.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Out of the chamber [of the south] cometh the storm: and cold out of the north.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
By the breath of God ice is given: and the breadth of the waters is straitened.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
Yea, he ladeth the thick cloud with moisture; he spreadeth abroad the cloud of his lightning:
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
And it is turned round about by his guidance, that they may do whatsoever he commandeth them upon the face of the habitable world.
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
Whether it be for correction, or for his land, or for mercy, that he cause it to come.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Hearken unto this, O Job: stand still, and consider the wondrous works of God.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
Dost thou know how God layeth [his charge] upon them, and causeth the lightning of his cloud to shine?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
Dost thou know the balancings of the clouds, the wondrous works of him which is perfect in knowledge?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
How thy garments are warm, when the earth is still by reason of the south [wind]?
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
Canst thou with him spread out the sky, which is strong as a molten mirror?
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Teach us what we shall say unto him; [for] we cannot order [our speech] by reason of darkness.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
Shall it be told him that I would speak? or should a man wish that he were swallowed up?
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
And now men see not the light which is bright in the skies: but the wind passeth, and cleanseth them.
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
Out of the north cometh golden splendour: God hath upon him terrible majesty.
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
[Touching] the Almighty, we can not find him out; he is excellent in power: and in judgment and plenteous justice he will not afflict.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Men do therefore fear him: he regardeth not any that are wise of heart.

< Ayubu 37 >