< Ayubu 36 >

1 Elihu aliendelea na kusema,
Elihu also continued, and said,
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
"Bear with me a little, and I will show you; for I still have something to say on God's behalf.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will get my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For truly my words are not false. One who is perfect in knowledge is with you.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
"Look, God is mighty, and doesn't despise anyone. He is mighty in strength of understanding.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He doesn't preserve the life of the wicked, but gives to the afflicted their right.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He doesn't withdraw his eyes from the righteous, but with kings on the throne, he sets them forever, and they are exalted.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
If they are bound in fetters, and are taken in the cords of afflictions,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
then he shows them their work, and their transgressions, that they have behaved themselves proudly.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
He also opens their ears to instruction, and commands that they return from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they listen and serve him, they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
But if they do not listen, they shall perish by the sword; they shall die without knowledge.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
"But those who are godless in heart lay up anger. They do not cry for help when he binds them.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
They die in youth. Their life perishes among the unclean.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
He delivers the afflicted by their affliction, and opens their ear in oppression.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Yes, he would have allured you out of distress, into a broad place, where there is no restriction. That which is set on your table would be full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
"But you are full of the judgment of the wicked. Judgment and justice take hold of you.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Do not let riches entice you to wrath, neither let the great size of a bribe turn you aside.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Would your wealth sustain you in distress, or all the might of your strength?
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Do not desire the night, when people are cut off in their place.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Take heed, do not regard iniquity; for you have chosen this rather than affliction.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Look, God is exalted in his power. Who is a teacher like him?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who has prescribed his way for him? Or who can say, 'You have committed unrighteousness?'
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
"Remember that you magnify his work, whereof men have sung.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
All men have looked thereon. Man sees it afar off.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
Look, God is great, and we do not know him. The number of his years is unsearchable.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
For he draws up the drops of water, which distill in rain from his vapor,
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
Which the skies pour down and which drop on humankind abundantly.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Yes, can any understand the spreading of the clouds, and the thunderings of his pavilion?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
Look, he spreads his light around him. He covers the bottom of the sea.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
For by these he judges the people. He gives food in abundance.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
He covers his hands with the lightning, and commands it to strike the mark.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
Its noise tells about him, and the livestock also concerning the storm that comes up.

< Ayubu 36 >