< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Elihu mówił dalej:
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Słuchajcie, mądrzy, moich słów i wy, uczeni, posłuchajcie mnie.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
Ucho bowiem bada słowa, jak podniebienie smakuje pokarm.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Wybierzmy sobie sąd, rozeznajmy między sobą, co jest dobre.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
Hiob bowiem powiedział: Jestem sprawiedliwy, a Bóg odrzucił moją sprawę.
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Czy mam kłamać wbrew swojej racji? Nieuleczalna jest moja rana, bez przestępstwa.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
Czy jest człowiek podobny do Hioba, który pije obelgi jak wodę?
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
I który obraca się w towarzystwie czyniących nieprawość i chodzi z niegodziwcami?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
Powiedział bowiem: Nic to nie pomoże człowiekowi, że ma upodobanie w Bogu.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Dlatego posłuchajcie mnie, ludzie rozumni: Daleki jest Bóg od niegodziwości, Wszechmocny – od nieprawości.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
Bo odpłaci człowiekowi według jego czynu i wynagrodzi każdemu według jego drogi.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Nie, naprawdę Bóg nie czyni przewrotnie, Wszechmocny nie wypacza sądu.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Któż mu powierzył ziemię? Kto urządził cały okrąg świata?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
Gdyby zwrócił ku człowiekowi swoje serce, gdyby wziął do siebie jego ducha i tchnienie;
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
To zginęłoby wszelkie ciało razem, a człowiek w proch by się obrócił.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
Jeśli więc masz rozum, posłuchaj tego [i] nadstaw uszu na moje słowa.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Czy ma panować ten, który nienawidzi prawości? Czy potępisz tego, który jest bardzo sprawiedliwy?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Czy wypada do króla mówić: Nikczemniku? A do książąt: Bezbożni?
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
Tym bardziej do tego, który nie ma względu na książąt i nie stawia bogacza nad ubogim? Oni wszyscy bowiem są dziełem jego rąk.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
Umrą nagle, o północy lud będzie wzruszony i przeminie, a mocarz zostanie usunięty bez [udziału] ręki [ludzkiej].
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
Jego oczy bowiem patrzą na drogi człowieka i [on] widzi wszystkie jego kroki.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
Nie ma ciemności ani cienia śmierci, gdzie mogliby się ukryć ci, którzy czynią nieprawość.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
Na człowieka bowiem nie wkłada więcej [niż to, co słuszne], aby stawił się na sąd przed Bogiem.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
Rozbije wielu mocarzy i innych osadzi w ich miejsce.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
A ponieważ zna ich czyny, wywraca ich w nocy, aby byli zmiażdżeni.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
Chłoszcze ich jako niegodziwych w miejscu widocznym;
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Za to, że odstąpili od niego i nie zważali na żadne jego drogi;
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
Z tego powodu dochodzi do niego wołanie biednych, a on wysłuchuje wołania ubogich.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
Gdy zaprowadzi pokój, któż go zburzy? A gdy zakryje swoje oblicze, któż go ujrzy? [A czyni] tak zarówno narodowi, jak i człowiekowi;
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
Aby obłudnik już nie panował i nie był pułapką dla ludzi.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
Doprawdy, powinieneś mówić do Boga: Poniosłem [karę], a nie będę [już] grzeszyć.
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
Naucz mnie tego, [czego] nie widzę; jeśli popełniłem nieprawość, [już] więcej tego nie uczynię.
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Czy [wszystko] ma być po twojej myśli? On odpłaci, czy odrzucisz, czy wybierzesz, a nie ja. Ale jeśli wiesz lepiej, to powiedz.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Niech mi powiedzą ludzie rozumni, niech człowiek mądry posłucha mnie:
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Hiob mówi niemądrze, a jego słowa nie są roztropne.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Niech Hiob zostanie doświadczony do końca za swoje odpowiedzi odnośnie do niegodziwych ludzi.
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
Dodaje bowiem buntu do swego grzechu, klaszcze przy nas rękoma i mnoży swoje słowa przeciwko Bogu.

< Ayubu 34 >