< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
Moreover Elihu answered and said,
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Hear my words, ye wise men; and give ear unto me, ye that have knowledge.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
For the ear trieth words, as the palate tasteth meat.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Let us choose for us that which is right: let us know among ourselves what is good.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
For Job hath said, I am righteous, and God hath taken away my right:
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Notwithstanding my right I am [accounted] a liar; my wound is incurable, [though I am] without transgression.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
What man is like Job, who drinketh up scorning like water?
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
Which goeth in company with the workers of iniquity, and walketh with wicked men.
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
For he hath said, it profiteth a man nothing that he should delight himself with God.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Therefore hearken unto me, ye men of understanding: far be it from God, that he should do wickedness; and from the Almighty, that he should commit iniquity.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
For the work of a man shall he render unto him, and cause every man to find according to his ways.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Yea, of a surety, God will not do wickedly, neither will the Almighty pervert judgment.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Who gave him a charge over the earth? or who hath disposed the whole world?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
If he set his heart upon man, [if] he gather unto himself his spirit and his breath;
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
All flesh shall perish together, and man shall turn again unto dust.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
If now [thou hast] understanding, hear this: hearken to the voice of my words.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
Shall even one that hateth right govern? and wilt thou condemn him that is just [and] mighty?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
Is it [fit] to say to a king, [Thou art] vile? [or] to nobles, [Ye are] wicked?
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
[How much less to] him that respecteth not the persons of princes, nor regardeth the rich more than the poor? for they all are the work of his hands.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
In a moment they die, even at midnight; the people are shaken and pass away, and the mighty are taken away without hand.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
For his eyes are upon the ways of a man, and he seeth all his goings.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
There is no darkness, nor shadow of death, where the workers of iniquity may hide themselves.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
For he needeth not further to consider a man, that he should go before God in judgment.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
He breaketh in pieces mighty men [in ways] past finding out, and setteth others in their stead.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
Therefore he taketh knowledge of their works; and he overturneth them in the night, so that they are destroyed.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
He striketh them as wicked men in the open sight of others;
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Because they turned aside from following him, and would not have regard to any of his ways:
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
So that they caused the cry of the poor to come unto him, and he heard the cry of the afflicted.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
When he giveth quietness, who then can condemn? and when he hideth his face, who then can behold him? whether [it be done] unto a nation, or unto a man, alike:
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
That the godless man reign not, that there be none to ensnare the people.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
For hath any said unto God, I have borne [chastisement], I will not offend [any more]:
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
That which I see not teach thou me: if I have done iniquity, I will do it no more?
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
Shall his recompence be as thou wilt, that thou refusest it? for thou must choose, and not I: therefore speak what thou knowest.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Men of understanding will say unto me, yea, every wise man that heareth me:
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Job speaketh without knowledge, and his words are without wisdom.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
Would that Job were tried unto the end, because of his answering like wicked men.
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
For he addeth rebellion unto his sin, he clappeth his hands among us, and multiplieth his words against God.

< Ayubu 34 >