< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Audi igitur Iob eloquia mea, et omnes sermones meos ausculta.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Ecce aperui os meum, loquatur lingua mea in faucibus meis.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Simplici corde meo sermones mei, et sententiam puram labia mea loquentur.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
Spiritus Dei fecit me, et spiraculum Omnipotentis vivificavit me.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Si potes, responde mihi, et adversus faciem meam consiste.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Ecce, et me sicut et te fecit Deus, et de eodem luto ego quoque formatus sum.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Verumtamen miraculum meum non te terreat, et eloquentia mea non sit tibi gravis.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Dixisti ergo in auribus meis, et vocem verborum tuorum audivi:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Mundus sum ego, et absque delicto: immaculatus, et non est iniquitas in me.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Quia querelas in me reperit, ideo arbitratus est me inimicum sibi.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Posuit in nervo pedes meos, custodivit omnes semitas meas.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Hoc est ergo, in quo non es iustificatus: respondebo tibi, quia maior sit Deus homine.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Adversus eum contendis quod non ad omnia verba responderit tibi?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Semel loquitur Deus, et secundo idipsum non repetit.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
Per somnium in visione nocturna, quando irruit sopor super homines, et dormiunt in lectulo:
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Tunc aperit aures virorum, et erudiens eos instruit disciplina,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
Ut avertat hominem ab his, quæ facit, et liberet eum de superbia:
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
Eruens animam eius a corruptione: et vitam illius, ut non transeat in gladium.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
Increpat quoque per dolorem in lectulo, et omnia ossa eius marcescere facit.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
Abominabilis ei fit in vita sua panis, et animæ illius cibus ante desiderabilis.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Tabescet caro eius, et ossa, quæ tecta fuerant, nudabuntur.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Appropinquavit corruptioni anima eius, et vita illius mortiferis.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Si fuerit pro eo Angelus loquens, unus de millibus, ut annuntiet hominis æquitatem:
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Miserebitur eius, et dicet: Libera eum, ut non descendat in corruptionem: inveni in quo ei propitier.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Consumpta est caro eius a suppliciis, revertatur ad dies adolescentiæ suæ.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Deprecabitur Deum, et placabilis ei erit: et videbit faciem eius in iubilo, et reddet homini iustitiam suam.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Respiciet homines, et dicet: Peccavi, et vere deliqui, et, ut eram dignus, non recepi.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
Liberavit animam suam ne pergeret in interitum, sed vivens lucem videret.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Ecce, hæc omnia operatur Deus tribus vicibus per singulos:
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
Ut revocet animas eorum a corruptione, et illuminet luce viventium.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Attende Iob, et audi me: et tace, dum loquor.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Si autem habes quod loquaris, responde mihi, loquere: volo enim, te apparere iustum.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Quod si non habes, audi me: tace, et docebo te sapientiam.

< Ayubu 33 >