< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Then was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the family of Ram; against Job was his wrath kindled, because he justified himself rather than God.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
Also against his three friends was his wrath kindled, because they had found no answer, and yet had condemned Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Now Elihu had waited to speak unto Job, because they were older than he.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
And when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, his wrath was kindled.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
And Elihu the son of Barachel the Buzite answered and said: I am young, and ye are very old; wherefore I held back, and durst not declare you mine opinion.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
I said: 'Days should speak, and multitude of years should teach wisdom.'
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
But it is a spirit in man, and the breath of the Almighty, that giveth them understanding.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
It is not the great that are wise, nor the aged that discern judgment.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Therefore I say: 'Hearken to me; I also will declare mine opinion.'
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Behold, I waited for your words, I listened for your reasons, whilst ye searched out what to say.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
Yea, I attended unto you, and, behold, there was none that convinced Job, or that answered his words, among you.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
Beware lest ye say: 'We have found wisdom; God may vanquish him, not man!'
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
For he hath not directed his words against me; neither will I answer him with your speeches.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
They are amazed, they answer no more; words are departed from them.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
And shall I wait, because they speak not, because they stand still, and answer no more?
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
I also will answer my part, I also will declare mine opinion.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
For I am full of words; the spirit within me constraineth me.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Behold, mine inwards are as wine which hath no vent; like new wine-skins which are ready to burst.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
I will speak, that I may find relief; I will open my lips and answer.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
Let me not, I pray you, respect any man's person; neither will I give flattering titles unto any man.
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
For I know not to give flattering titles; else would my Maker soon take me away.

< Ayubu 32 >