< Ayubu 31 >

1 Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
Hice un pacto con mis ojos. ¿Cómo podría entonces fijar mi mirada en una doncella?
2 Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
¿Cuál sería la recompensa de ʼEloah desde arriba o la herencia de ʼEL-Shadday desde las alturas?
3 Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
¿No es la calamidad para el perverso, y el desastre para los que obran iniquidad?
4 Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
¿No observa Él mis caminos y cuenta todos mis pasos?
5 Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
Si anduve con vanidad y mi pie se apresuró al engaño,
6 na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
sea yo pesado en balanza justa, y conozca ʼEloah a mi integridad.
7 Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
Si mi paso se apartó del camino, mi corazón se fue tras mis ojos o si alguna mancha se pegó a mis manos,
8 na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
siembre yo y coma otro. Sea arrancada mi cosecha.
9 Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
Si mi corazón fue seducido por una mujer y aceché a la puerta de mi prójimo,
10 na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
muela mi esposa para otro y sobre ella se encorven otros.
11 Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
Porque eso sería una lujuriosa perversidad y una iniquidad castigada por los jueces,
12 Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
un fuego que consume hasta el Abadón, que arrancaría toda mi hacienda.
13 Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
Si menosprecié el derecho de mi esclavo o de mi esclava, cuando ellos tenían una queja contra mí,
14 kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
¿qué haré cuando ʼEL me levante? ¿Qué le responderé cuando me llame a cuentas?
15 Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
El que me formó en el vientre, ¿no lo formó también a él? ¿No nos formó el mismo en la matriz?
16 kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
Si estorbé el anhelo de los pobres o hice desfallecer los ojos de la viuda,
17 au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
o comí mi bocado a solas y el huérfano no comió de él,
18 kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
aunque desde mi juventud creció conmigo como con un padre y lo guié desde el seno materno,
19 ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
si vi a algún vagabundo sin ropas o algún menesteroso sin algo con lo cual cubrirse,
20 ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
y sus órganos internos no me bendijeron al calentarse con el vellón de mis ovejas,
21 ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
si alcé mi mano contra el huérfano cuando me vi apoyado en la puerta,
22 Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
despréndase mi brazo del hombro y descoyúntese mi brazo de su hueso.
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
Porque temo el castigo de ʼEL, pues ante su majestad nada puedo hacer.
24 Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
Si fijé mi confianza en el oro y al metal precioso dije: Tú eres mi esperanza,
25 na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
si me complací por mis grandes riquezas y porque mi mano ganó mucho,
26 Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
si miré al sol resplandeciente o a la luna que se desplazaba en su esplendor,
27 na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
si mi corazón fue seducido en secreto y mi boca les envió un beso con la mano,
28 hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
también sería iniquidad digna de castigo, por negar al ʼEL que está en lo alto.
29 Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
¿Me alegré de la ruina del que me aborrecía o salté de júbilo porque el mal cayó sobre él?
30 Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
¡No! Nunca dejé que mi boca pecara, ni al maldecir al enemigo, ni al hacer una imprecación para que muriera.
31 Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
Decían los esclavos de mi casa: ¿Quién no se sació con su carne?
32 (hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
El forastero no pasaba la noche en la calle. Yo abría mis puertas al viajero.
33 Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
Si encubrí mis transgresiones como Adán y oculté la iniquidad en mi seno
34 kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
por temor a la muchedumbre, o porque el desprecio de la gente me intimidó y no salí a la puerta.
35 Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
¡Ojalá me escuchara! ¡Ciertamente aquí está mi firma! ¡Que ʼEL-Shadday me responda!
36 Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
Ciertamente lo llevaría sobre mi hombro y me lo ataría a la cabeza como una corona.
37 Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
Le rendiría cuenta de todos mis pasos, y como a un príncipe me acercaría ante Él.
38 Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
Si mi tierra clama contra mí y lloran sus surcos junto a ella,
39 ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
si comí su fruto sin pagar o afligí a sus labradores,
40 ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.
crezcan abrojos en lugar de trigo y cizaña en vez de cebada. Aquí terminan las palabras de Job.

< Ayubu 31 >