< Ayubu 30 >

1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
“Mas ahora se ríen de mí los que tienen menos años que yo, a cuyos padres yo hubiera desdeñado de tomar como perros para mi ganado.
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Aun la fuerza de sus manos ¿de qué me habría servido? ya que carecen ellos de todo vigor.
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
Muertos de miseria y de hambre roen el yermo, la tierra desolada y vacía.
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Recogen frutos amargos de arbustos, y se sustentan con raíces de retama.
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
Expulsados de la sociedad, y perseguidos con gritos habitan como ladrones,
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
en los barrancos de los torrentes, en las cuevas de la tierra y en las breñas.
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
Entre la maleza lanzan sus gritos, y se reúnen bajo las zarzas.
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
Son hombres insensatos, hijos de gente sin nombre, echados del país a viva fuerza.
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
Y ahora soy escarnecido por ellos y el objeto de sus pullas.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
Me abominan, se apartan de mí; y no se avergüenzan de escupirme en la cara.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
Han perdido todo freno, me humillan y pierden todo respeto en mi presencia.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
A mi derecha se levanta el populacho; hacen vacilar mis pies; traman contra mí maquinaciones para perderme.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
Me cortan el camino, procuran mi caída; nadie me presta auxilio contra ellos.
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
Como por brecha ancha irrumpen, se revuelcan entre los escombros.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
Me han acometido terrores, y como el viento se llevan mi nobleza; cual nube pasó mi prosperidad.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
Ahora mi vida se derrama dentro de mí, se han apoderado de mí días aciagos.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
La noche me taladra los huesos, y no me dan tregua los que me roen.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
Su gran muchedumbre ha desfigurado mi vestido; me ciñen como el cabezón de mi túnica.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
Me han echado en el lodo, soy como el polvo y la ceniza.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
A Ti clamo por auxilio, y Tú no me respondes; permanezco en pie, y Tú me miras (con indiferencia).
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
Te has tornado para mí en enemigo, y me persigues con todo tu poder.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
Me alzas sobre el viento, y me haces cabalgar; me sacudes sin darme sostén.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
Porque bien sé que me entregarás a la muerte, a la casa adonde van a parar todos los vivientes.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Sin embargo el que va a perecer ¿no extiende su mano? en su aflicción ¿no pide auxilio?
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
¿No lloraba yo con el atribulado? ¿no se afligía mi alma por el pobre?
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
Pero esperando el bien, me vino el mal; aguardando la luz he quedado cubierto de tinieblas.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
Mis entrañas se abrazan sin descanso; me han sobrevenido días de aflicción.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
Ando como quien está de luto, sin alegría, me levanto en la asamblea para clamar por auxilio.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
Soy ahora hermano de los chacales, y compañero de los avestruces.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
Ennegrecida se me cae la piel, y mis huesos se consumen por la fiebre.
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
El son de mi cítara se ha trocado en lamentos, y mi flauta en voz de llanto.”

< Ayubu 30 >