< Ayubu 30 >

1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
And now, laughed at me, Have the younger in days than I, Whose fathers I have loathed to set With the dogs of my flock.
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
Also — the power of their hands, why [is it] to me? On them hath old age perished.
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
With want and with famine gloomy, Those fleeing to a dry place, Formerly a desolation and waste,
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
Those cropping mallows near a shrub, And broom-roots [is] their food.
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
From the midst they are cast out, (They shout against them as a thief),
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
In a frightful place of valleys to dwell, Holes of earth and clefts.
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
Among shrubs they do groan, Under nettles they are gathered together.
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
Sons of folly — even sons without name, They have been smitten from the land.
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
And now, their song I have been, And I am to them for a byword.
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
They have abominated me, They have kept far from me, And from before me have not spared to spit.
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
Because His cord He loosed and afflicteth me, And the bridle from before me, They have cast away.
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
On the right hand doth a brood arise, My feet they have cast away, And they raise up against me, Their paths of calamity.
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
They have broken down my path, By my calamity they profit, 'He hath no helper.'
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
As a wide breach they come, Under the desolation have rolled themselves.
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
He hath turned against me terrors, It pursueth as the wind mine abundance, And as a thick cloud, Hath my safety passed away.
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
And now, in me my soul poureth itself out, Seize me do days of affliction.
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
At night my bone hath been pierced in me, And mine eyelids do not lie down.
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
By the abundance of power, Is my clothing changed, As the mouth of my coat it doth gird me.
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
Casting me into mire, And I am become like dust and ashes.
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
I cry unto Thee, And Thou dost not answer me, I have stood, and Thou dost consider me.
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
Thou art turned to be fierce to me, With the strength of Thy hand, Thou oppressest me.
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
Thou dost lift me up, On the wind Thou dost cause me to ride, And Thou meltest — Thou levellest me.
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
For I have known To death Thou dost bring me back, And [to] the house appointed for all living.
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
Surely not against the heap Doth He send forth the hand, Though in its ruin they have safety.
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
Did not I weep for him whose day is hard? Grieved hath my soul for the needy.
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
When good I expected, then cometh evil, And I wait for light, and darkness cometh.
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
My bowels have boiled, and have not ceased, Gone before me have days of affliction.
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
Mourning I have gone without the sun, I have risen, in an assembly I cry.
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
A brother I have been to dragons, And a companion to daughters of the ostrich.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
My skin hath been black upon me, And my bone hath burned from heat,
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
And my harp doth become mourning, And my organ the sound of weeping.

< Ayubu 30 >